Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Constantine John Kanyasu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Geita Mjini

Primary Question

MHE. CONSTANTINE J. KANYASU aliuliza:- Je, hasara na faida gani Taifa linapata kuwa uchumi wa kati na asilimia ngapi ya wananchi wanafahamu na kuishi uchumi wa kati?

Supplementary Question 1

MHE. CONSTANTINE J. KANYASU: Mheshimiwa Spika, namshukuru Waziri kwa majibu mazuri. Naomba kuuliza maswali mawili ya nyongeza:-

Mheshimiwa Spika, kwa kuwa, Tanzania ilipoingia kwenye uchumi wa kati wa chini, baadaye lilikuja tatizo la Corona na sasa hivi tuna-experience mgogoro wa kivita wa Ukraine; dunia inatabiriwa kuwa na mgogoro mwingine wa kiuchumi; Tanzania itaathirika vipi iwapo mgogoro huo utatokea? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, lakini swali langu la pili, katika jibu lake la swali langu la msingi Mheshimiwa Naibu Waziri amesema moja ya sifa ya nchi inapoingia kwenye uchumi wa kati ni kuwa na sifa ya kukopeshwa mikopo ya kibiashara. Hata hivyo zimekuwepo lawama baada ya Tanzania kukopa kibiashara: Ni nini mtazamo wa Wizara iwapo tutaendelea kukopa kibiashara wakati wengine wanaona pamoja na sifa hiyo tunayo, tusikope kibiashara? (Makofi)

Name

Hamad Hassan Chande

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kojani

Answer

NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO: Mheshimiwa Spika, ahsante. Kwa niaba ya Waziri wa Fedha na Mipango naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Constantine John Kanyasu, Mbunge wa Geita Mjini, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, kwanza naomba nimhakikishie Mbunge kwamba, nchi yetu bado haijashuka katika uchumi wa kati chini, bado tuko pale pale. Pamoja na changamoto zote hizo, kilichotokea ni kushuka kwa uchumi wa mtu mmoja mmoja tukatoka 7% kuja 4.8%.

Mheshimiwa Spika, lakini swali lake la pili, kauli ya Serikali ni kwamba wananchi waache kuwa na lawama kwa sababu Serikali yao iko makini sana katika kufanya tathmini aina gani ya mkopo nchi yetu iingie, na una tija gani kwa maslahi ya Taifa letu?