Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 15 Sitting 14 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 181 2024-04-25

Name

Sebastian Simon Kapufi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mpanda Mjini

Primary Question

MHE. DKT. CHRISTINA C. MNZAVA K.n.y. MHE. SEBASTIAN S. KAPUFI aliuliza:-

Je, ni lini Serikali itapeleka mashine ya X-ray katika Hospitali ya Manispaa ya Mpanda?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE) alijibu:-

Mheshimiwa Spika, Serikali inaendelea kuboresha huduma za uchunguzi za radiolojia kwa kusimika mashine za X-ray na ultrasound katika Vituo vya Kutolea Huduma za Afya ya Msingi nchini. Katika kipindi cha mwaka wa fedha 2021/2022 hadi 2022/2024, jumla ya mashine 280 za kidigitali za X-ray na mashine za ultrasound 322 zimenunuliwa na kusimikwa katika Vituo vya kutolea Huduma za Afya ya Msingi.

Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2022/2023, Serikali imepeleka mashine tatu za X-ray katika Mkoa wa Katavi ambapo zimefungwa katika Halmashauri ya Mpimbwe, Mlele, Nsimbo. Aidha, Hospitali ya Halmashauri ya Manispaa ya Mpanda iko kwenye orodha ya vituo vitakavyopelekewa mashine za X-ray awamu inayofuata.