Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Dr. Christina Christopher Mnzava

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DKT. CHRISTINA C. MNZAVA K.n.y. MHE. SEBASTIAN S. KAPUFI aliuliza:- Je, ni lini Serikali itapeleka mashine ya X-ray katika Hospitali ya Manispaa ya Mpanda?

Supplementary Question 1

MHE. DKT. CHRISTINA C. MNZAVA: Mheshimiwa Spika, Mheshimiwa Kapufi anashukuru sana kwa jitihada ambazo zinafanywa na Serikali, lakini, nina swali moja la nyongeza, Kituo cha Afya cha Ushetu kimeboreshwa na kimekarabatiwa lakini hakina digital X-ray. Je, ni lini Serikali itapeleka digital X-ray katika Kituo cha Afya cha Ushetu, kilichopo Jimbo la Ushetu?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, ni kweli kwamba Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kutambua uhitaji wa huduma za afya katika Kata ya Ushetu ilikarabati Kituo cha Afya cha Ushetu. Nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge, kwamba tunaelekea kupeleka mashine ya digital X-ray kwenye vituo vyote vilivyopanuliwa na kujengewa majengo ya X-ray kikiwemo Kituo hiki cha Ushetu. Ahsante sana.

Name

Martha Festo Mariki

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DKT. CHRISTINA C. MNZAVA K.n.y. MHE. SEBASTIAN S. KAPUFI aliuliza:- Je, ni lini Serikali itapeleka mashine ya X-ray katika Hospitali ya Manispaa ya Mpanda?

Supplementary Question 2

MHE. MARTHA F. MARIKI: Mheshimiwa Spika, Wilaya ya Tanganyika hatuna kabisa mtaalamu wa X-ray. Je, ni lini Serikali itapeleka mtaalamu huyo ili kuwasaidia wananchi waweze kupata huduma zilizokusudiwa? Nakushukuru.

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, kumekuwa na upungufu wa Wataalam wa X-ray na Ultrasound kwenye vituo vyetu vya huduma hususani ngazi ya afya ya msingi. Ofisi ya Rais, TAMISEMI tayari tumeshaanza kutoa mafunzo ya muda mfupi kwa Wataalam wa X-Ray na Ultrasound ili kuhakikisha kwamba hospitali zote zenye mashine hizo zinapata wataalam kwa ajili ya huduma hiyo. Kwa hiyo, naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba Kituo hicho cha Afya lakini pia Halmashauri ya Tanganyika itapelekewa Wataalam wa X-Ray na Ultrasound ili kuhakikisha kwamba huduma zinatolewa vizuri, ahsante sana.

Name

Neema Gerald Mwandabila

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DKT. CHRISTINA C. MNZAVA K.n.y. MHE. SEBASTIAN S. KAPUFI aliuliza:- Je, ni lini Serikali itapeleka mashine ya X-ray katika Hospitali ya Manispaa ya Mpanda?

Supplementary Question 3

MHE. NEEMA G. MWANDABILA: Mheshimiwa Spika, nataka kufahamu, ni lini Wizara itapeleka X-Ray katika Kituo cha Kamsamba? Ahsante.

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, mpango wa Serikali ni kuhakikisha kwamba baada ya hivi vituo vya afya kukamilika na kujengewa majengo maalum ya X-ray vinatafutiwa fedha na kupelekewa vifaa vya X-ray kwa maana ya mashine za X-ray kwa ajili ya huduma hizo. Kwa hiyo, naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba baada ya kukamilisha jengo la X-ray tutahakikisha tunatafuta fedha kwa ajili ya kupeleka mashine ya X-ray, ahsante sana.

Name

Esther Lukago Midimu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DKT. CHRISTINA C. MNZAVA K.n.y. MHE. SEBASTIAN S. KAPUFI aliuliza:- Je, ni lini Serikali itapeleka mashine ya X-ray katika Hospitali ya Manispaa ya Mpanda?

Supplementary Question 4

MHE. ESTHER L. MIDIMU: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi ili niweze kuuliza swali la nyongeza. Hospitali za Wilaya za Mkoa wa Simiyu tumepata mashine za X-ray, lakini hatuna wataalam, je, ni lini Serikali itatuletea wataalam wa X-Ray?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, ni kweli kwamba Mkoa wa Simiyu na halmashauri zake ni moja ya mikoa ambayo ina upungufu mkubwa wa Wataalamu wa Huduma za Mionzi ikiwemo X-Ray na Ultrasound. Nimhakikishie tu kwenye kibali cha ajira ambacho kitatangazwa hivi karibuni tutaupa kipaumbele Mkoa wa Simiyu pamoja na halmashauri zake kupata wataalam wa X-Ray, ahsante sana. (Makofi)

Name

Shabani Hamisi Taletale

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Morogoro Kusini Mashariki

Primary Question

MHE. DKT. CHRISTINA C. MNZAVA K.n.y. MHE. SEBASTIAN S. KAPUFI aliuliza:- Je, ni lini Serikali itapeleka mashine ya X-ray katika Hospitali ya Manispaa ya Mpanda?

Supplementary Question 5

MHE. HAMISI S. TALETALE: Mheshimiwa Spika, ni lini Serikali italeta huduma ya X-ray katika Kituo cha Afya cha Mkuyuni? Ahsante.

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, nafahamu kwamba Kituo cha Afya cha Mkuyuni bado hakina jengo la X-ray na majengo haya ni maalum kwa sababu mashine zile ni mashine za mionzi. Kwa hiyo, nitumie nafasi hii kumwelekeza Mkurugenzi wa Halmashauri ya Morogoro kutenga fedha kwa ajili ya kuanza ujenzi wa jengo maalum kwa ajili ya mashine ya X-ray na baada ya kukamilisha tutapeleka mashine ya X-ray kwa ajili ya huduma hizo. Ahsante sana. (Makofi)