Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 15 Sitting 4 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 40 2024-04-05

Name

Benaya Liuka Kapinga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbinga Vijijini

Primary Question

MHE. BENAYA L. KAPINGA aliuliza:-

Je, lini Serikali itakamilisha ujenzi wa Shule za Sekondari katika Kata za Ngima, Mhongozi na Muungano - Halmashauri ya Mbinga?

Name

Zainab Athuman Katimba

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. ZAINAB A. KATIMBA) alijibu:-

Mheshimiwa Spika, Serikali inatambua kuwa Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga ina Kata tatu za Muungano, Ngima na Mhongozi ambazo hazina shule za sekondari. Aidha, Kupitia Mpango wa Kuboresha Elimu ya Sekondari (SEQUIP), halmashauri itaendelea kujenga Shule ya Kata ya Muungano (SEQUIP), awamu ya tatu ambapo ilitengewa shilingi milioni 560 katika bajeti ya mwaka 2023/2024.

Mheshimiwa Spika, katika bajeti ya mwaka 2024/2025, Kata ya Mhongozi imetengewa shilingi milioni 560 kwa ajili ya kujenga shule katika kata hiyo kupitia mpango wa kuboresha elimu ya sekondari awamu ya nne. Aidha, Kata ya Ngima itatengewa fedha katika bajeti ya Mwaka wa Fedha 2025/2026 ili kukamilisha ujenzi wa shule za kata katika Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga. (Makofi)