Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Benaya Liuka Kapinga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbinga Vijijini

Primary Question

MHE. BENAYA L. KAPINGA aliuliza:- Je, lini Serikali itakamilisha ujenzi wa Shule za Sekondari katika Kata za Ngima, Mhongozi na Muungano - Halmashauri ya Mbinga?

Supplementary Question 1

MHE. BENAYA L. KAPINGA: Mheshimiwa Spika, ahsante na nashukuru kwa majibu mazuri ya Serikali, hata hivyo, nina maswali madogo mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Spika, swali la kwanza; hii Kata ya Ngima wananchi kwa kushirikiana na mimi Mbunge tumejenga tayari madarasa manne. Je, Serikali iko tayari kutenga fedha japo kidogo kukamilisha madarasa haya ili yaweze kutumika mwakani Januari?

Mheshimiwa Spika, swali la pili; wananchi wa Kata ya Matiri pamoja na Kata ya Nguzo nao wamejenga Shule ya Sekondari Nguzo pamoja na Benaya Sekondari hazina miundombinu ya kutosha. Je, Serikali iko tayari kupeleka fedha kukamilisha miundombinu ya shule hizi?

Name

Zainab Athuman Katimba

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. ZAINAB A. KATIMBA): Mheshimiwa Spika, Serikali ina nia ya kuendelea kuboresha miundombinu ya shule na hivyo kwa kadri ya upatikanaji wa fedha Serikali itaweza kujenga madarasa hayo aliyoyataja Mheshimiwa Mbunge. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kuhusiana na swali lake la pili, Serikali inatambua jitihada ambazo zimefanywa na wananchi wa Mbinga DC za kujenga Shule ya Sekondari ya Benaya na Nguzo na shule hizo tayari zimeshasajiliwa na zina wanafunzi mpaka kidato cha pili. Kwa kuzingatia miundombinu ambayo bado haijakamilika katika shule hizo, Serikali kupitia bajeti ya halmashauri ya 2024/2025 imepanga kutumia shilingi milioni 62.5 kwa ajili ya shule hizo. Kwa hiyo, Serikali itaendelea kufanya tathmini ya ukamilishwaji wa miundombinu ya shule hizo ili kuongeza fedha kulingana na upatikanaji wake kwa ajili ya kuhakikisha kuwa ujenzi wa shule hizo unakamilishwa na kuunga mkono jitihada za wananchi. Ahsante. (Makofi)