Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 15 Sitting 15 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 190 2024-04-29

Name

Joseph Kasheku Musukuma

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Geita

Primary Question

MHE. JOSEPH K. MUSUKUMA aliuliza:-

Je, lini Serikali itatoa kipaumbele cha ujenzi wa nyumba za Watumishi wa Halmashauri mpya ikiwemo Geita DC?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE) alijibu:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuanzia mwaka wa fedha 2020/2021 hadi 2023/2024, Serikali imetoa shilingi bilioni 48.66 kwa ajili ya ujenzi wa nyumba 201 za Wakurugenzi na Wakuu wa Idara. Kati ya fedha hizo, shilingi bilioni 13.85 zilitolewa kwa halmashauri mpya 31 zilizohamisha makao makuu kwenda kwenye maeneo yao ya utawala ikiwemo Halmashauri ya Wilaya ya Geita iliyopokea shilingi milioni 390 kwa ajili ya ujenzi wa nyumba tatu za Wakuu wa Idara na moja ya Mkurugenzi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika mwaka wa fedha 2023/2024 Mamlaka za Serikali za Mitaa zimetengewa shilingi bilioni 1.30 kwa ajili ya ukamilishaji wa nyumba 24 za Wakurugenzi wa halmashauri na shilingi bilioni 6.72 kwa ajili ya ujenzi wa nyumba 35 za Wakuu wa Idara. Hadi kufikia Machi, 2024 jumla ya nyumba 97 za Wakurugenzi na Wakuu wa Idara zilikuwa zimekamilika. Serikali itaendelea kutenga bajeti kwa ajili ya ujenzi wa nyumba za watumishi katika Halmashauri ya Geita, ahsante.