Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Joseph Kasheku Musukuma

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Geita

Primary Question

MHE. JOSEPH K. MUSUKUMA aliuliza:- Je, lini Serikali itatoa kipaumbele cha ujenzi wa nyumba za Watumishi wa Halmashauri mpya ikiwemo Geita DC?

Supplementary Question 1

MHE. JOSEPH K. MUSUKUMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, namshukuru sana Mheshimiwa Waziri kwa majibu. Mimi sikuuliza swali la kisera, nimeuliza swali la jimbo langu. Ukitaja shilingi bilioni 44, kwanza unanichongea kwa wapiga kura wangu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali langu ni kwamba, kweli tumepokea fedha, shilingi milioni 150 kwa ajili ya ujenzi wa nyumba ya Mkurugenzi, lakini baadhi ya halmashauri tulizohamanazo, zile halmashauri 31 tulipewa shilingi milioni 150, wengine wameshaongeza shilingi milioni 300 mpaka shilingi milioni 350, unakuta nyumba za Wakurugenzi zina mpaka swimming pool, zina mageti, zina fence na kila kitu; lakini halmashauri yangu ina shilingi milioni 150. Ni lini utaongeza pesa ili tuwe na uwiano na wale uliowapelekea shilingi milioni 330? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, kama kwa miaka mitano tutajenga nyumba tatu kwa hizi halmashauri ambazo tulizirudisha vijijini, Wakuu wa Idara wapo 18, it means kuna miaka 30 huko mbele ili watu wetu wawe ndani. Ni lini Serikali itakubaliana na mawazo tunayoyatoa humu Bungeni kwamba yapo mashirika ya Serikali kama National House, Watumishi House ziingie mkataba na hizi halmashauri, kwani tuna uwezo wa kulipa hata kidogo kidogo ili waweze kujenga kwa mara moja tuepukane na hili suala la kupewa nyumba tatu kwa miaka mitano? (Makofi)

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Mwenyekiti, nianze tu kwa kumhakikishia Mheshimiwa Mbunge kwamba tumetoa taarifa kwa upana kwa maana ya sura ya kitaifa ili wananchi wajue kazi kubwa inayofanywa na Serikali yao katika ujenzi wa miundombinu ya nyumba za watumishi, lakini pia katika majengo ya utawala.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba tunatambua kuna baadhi ya halmashauri waliongezewa fedha kwa ajili ya ujenzi wa nyumba za Wakurugenzi au Wakuu wa Idara pale ambapo fedha haikutosha. Moja ya jukumu la Mkurugenzi ni kuwasilisha taarifa rasmi Ofisi ya Rais, TAMISEMI akielezea hatua iliyofikiwa baada ya kuanza utekelezaji na fedha kumalizika.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, nitumie nafasi hii kumwelekeza Mkurugenzi wa Halmashauri ya Geita awasilishe andiko linaloelezea hatua waliyofikia kwenye ujenzi na kiasi gani cha fedha kinahitajika ili Serikali iweze kuchukua hatua.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pili, Serikali ilishatoa maelekezo kwa Wakurugenzi wote wa Mamlaka za Serikali za Mitaa kutumia fursa za Watumishi Housing na National Housing kuingia mikataba na kukubaliana kujenga nyumba za Wakuu wa Idara na watumishi wengine ili waanze kulipa kwa awamu. Kwa hiyo, ni suala tu la wao kutekeleza, lakini Serikali ilishatoa maelekezo na kuna baadhi ya halmashauri ambazo tayari zilianza kutekeleza utaratibu huu, ahsante

Name

Shabani Omari Shekilindi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Lushoto

Primary Question

MHE. JOSEPH K. MUSUKUMA aliuliza:- Je, lini Serikali itatoa kipaumbele cha ujenzi wa nyumba za Watumishi wa Halmashauri mpya ikiwemo Geita DC?

Supplementary Question 2

MHE. SHABANI O. SHEKILINDI: Mheshimiwa Mwenyekiti, je, ni lini Serikali itajenga nyumba za watumishi hasa kada ya ualimu na kada ya afya katika Jimbo la Lushoto? Ahsante. (Makofi)

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali imeweka mpango mkakati wa kujenga nyumba za watumishi hususan wa sekta ya afya na elimu katika shule na katika vituo vyetu na utekelezaji umeshaanza. Shule nyingi zimeendelea kujengewa nyumba za walimu na pia vituo vya afya, hospitali na zahanati zinaendelea kujengwa. Nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba katika Jimbo lake la Lushoto tutahakikisha pia tunaendelea kutoa kipaumbele kuhakikisha kwamba nyumba hizo zinajengwa.

Name

Yustina Arcadius Rahhi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JOSEPH K. MUSUKUMA aliuliza:- Je, lini Serikali itatoa kipaumbele cha ujenzi wa nyumba za Watumishi wa Halmashauri mpya ikiwemo Geita DC?

Supplementary Question 3

MHE. YUSTINA A. RAHHI: Mheshimiwa Mwenyekiti, Halmashauri ya Wilaya ya Mbulu baada ya kugawana na Halmashauri ya Mji wa Mbulu, wamehamia katika mji wa Dongobesh na wamekamilisha jengo la utawala. Sasa ni lini Serikali itawajengea Watumishi wa Halmashauri ya Mbulu nyumba za kuishi? Nakushukuru sana.

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Mwenyekiti, nitumie nafasi hii kumkumbusha na kumsisitiza Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbulu kwamba waanze wao kupitia mapato ya ndani kutenga fedha kwa ajili ya kuanza ujenzi wa nyumba za watumishi wakati wakisubiri Serikali kwenda kuunga mkono na kukamilisha nyumba hizo, ahsante sana.

Name

Hussein Nassor Amar

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nyang'hwale

Primary Question

MHE. JOSEPH K. MUSUKUMA aliuliza:- Je, lini Serikali itatoa kipaumbele cha ujenzi wa nyumba za Watumishi wa Halmashauri mpya ikiwemo Geita DC?

Supplementary Question 4

MHE. HUSSEIN N. AMAR: Mheshimiwa Mwenyekiti, nianze kwa kuipongeza Serikali kwa kukamilisha ujenzi wa jengo la Halmashauri ya Nyang’hwale, lakini jengo lile ni zuri, kuna thamani nyingi iliyopo pale. Je, Serikali ipo tayari kutenga fedha kwa ajili ya kuweka uzio kwa ajili ya kulinda mali zote zilizo pale? (Makofi)

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali ipo tayari kuhakikisha inatenga fedha kwa ajili ya ujenzi wa uzio. Fedha hizo zinaweza zikatoka katika mapato ya ndani ya halmashauri, kwa hiyo, Mkurugenzi aanze kutekeleza hilo, lakini pia linaweza likatoka Serikali Kuu kwa awamu.