Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 15 Sitting 15 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 191 2024-04-29

Name

Hassan Seleman Mtenga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mtwara Mjini

Primary Question

MHE. YAHYA A. MHATA K.n.y. MHE. HASSAN S. MTENGA aliuliza: -

Je, lini Serikali itaongeza Walimu wa Masomo ya Sayansi kwa Shule za Sekondari Mtwara Mjini?

Name

Zainab Athuman Katimba

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. ZAINAB A. KATIMBA) alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Hassan Seleman Mtenga, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali imekuwa ikifanya jitihada kila mwaka kuajiri walimu wa masomo mbalimbali wakiwemo wa masomo ya Sayansi. Katika kipindi cha mwaka wa fedha 2020/2021 hadi mwaka 2022/2023, Serikali iliajiri walimu wa masomo ya Sayansi 8,425 ambapo Halmashauri ya Manispaa ya Mtwara Mikindani ilipata walimu 10.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mwaka 2023/2024 Serikali inatarajia kuajiri walimu 12,000 wa masomo mbalimbali wakiwemo wa sayansi ambao watapangiwa vituo vya kazi katika maeneo yenye upungufu mkubwa ikiwemo Manispaa ya Mtwara Mikindani.