Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Yahya Ally Mhata

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nanyumbu

Primary Question

MHE. YAHYA A. MHATA K.n.y. MHE. HASSAN S. MTENGA aliuliza: - Je, lini Serikali itaongeza Walimu wa Masomo ya Sayansi kwa Shule za Sekondari Mtwara Mjini?

Supplementary Question 1

MHE. YAHYA A. MHATA: Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na majibu mazuri ya Serikali, naomba kuuliza maswali mawili ya nyongeza. Halmashauri hii ya Manispaa ya Mtwara Mikindani kwa kweli ina changamoto kubwa sana. Mfano, hapa ninapozungumza kuna baadhi ya shule ina mwalimu mmoja tu wa chemistry, kuna baadhi ya shule ina mwalimu mmoja tu wa physics...

MWENYEKITI: Uliza swali.

MHE. YAHYA A. MHATA: Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali haioni kwamba wakati umefika, katika huu mgao wa walimu, Halmashauri hii ya Mtwara Mikindani ikapewa kipaumbele zaidi? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, nakwenda kwenye Halmashauri yangu ya Nanyumbu. Katika halmashauri hii, hali ndiyo mbaya zaidi ya huko. Hapa ninapozungumza, hata ufaulu wa wanafunzi ni mbaya. Mfano katika mitihani iliyopita kati ya wanafunzi 998 ni wanafunzi 19% tu ndiyo waliofaulu masomo ya sayansi. Je, Serikali haioni haja sasa kwa hii Mikoa ya Kusini ikapewa kipaumbele kupatiwa walimu wa sayansi ili vijana nao wapate haki ya kusoma masomo hayo? (Makofi)

Name

Zainab Athuman Katimba

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. ZAINAB A. KATIMBA): Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Mbunge, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu upungufu mkubwa wa walimu katika Halmashauri ya Manispaa ya Mtwara Mikindani, naomba kumpa taarifa Mheshimiwa Mbunge kwamba kama nilivyosema kwenye majibu yangu ya msingi, mwaka huu Serikali inatarajia kuajiri walimu 12,000. Sasa katika mgao huo, Serikali itaweka jicho la kipekee katika jimbo hili kwa ajili ya kuhakikisha kwamba walimu hao wanaweza kupatikana ili kupunguza upungufu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu swali la pili, naomba nimjibu Mheshimiwa Mbunge kwamba Serikali inafahamu umuhimu wa kuwa na walimu na hasa walimu wa masomo ya sayansi na kwa sababu Serikali tayari inaajiri walimu 12,000, kwa hiyo, itaangalia jimbo lako kwa jicho la pekee ili kuona kwamba walimu wanapatikana ili kupunguza ukali wa upungufu kwenye jimbo lako. (Makofi)

Name

Kenneth Ernest Nollo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bahi

Primary Question

MHE. YAHYA A. MHATA K.n.y. MHE. HASSAN S. MTENGA aliuliza: - Je, lini Serikali itaongeza Walimu wa Masomo ya Sayansi kwa Shule za Sekondari Mtwara Mjini?

Supplementary Question 2

MHE. KENNETH E. NOLLO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi nami niulize swali la nyongeza. Zipo halmashauri ambazo zina uwezo wa mapato na zina uwezo wa kuajiri walimu. Je, Serikali ina mpango gani wa kugatua suala la ajira ya walimu liende kwenye halmashauri ambazo wanaweza wakaajiri na wakaweza kuwalipa walimu badala ya kusubiri mgao wa kitaifa? Ahsante sana. (Makofi)

Name

Zainab Athuman Katimba

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. ZAINAB A. KATIMBA): Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Mbunge, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Ofisi ya Rais, TAMISEMI pamoja na mambo mengine inasimamia suala la ugatuzi kwa maana ya D by D na inapenda sana kuona halmashauri zinaweza kuwa na uwezo na ubunifu wa kutengeneza mapato makubwa ya ndani na kuweza kujiendesha zenyewe. Kwa hiyo, mawazo ya Mheshimiwa Mbunge ni mawazo mazuri, tunayachukua sisi kama Serikali, tutayachakata na tunaamini kwamba yataweza kutekelezeka.

Name

Dr. Oscar Ishengoma Kikoyo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Muleba kusini

Primary Question

MHE. YAHYA A. MHATA K.n.y. MHE. HASSAN S. MTENGA aliuliza: - Je, lini Serikali itaongeza Walimu wa Masomo ya Sayansi kwa Shule za Sekondari Mtwara Mjini?

Supplementary Question 3

MHE. DKT. OSCAR I. KIKOYO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru sana. Jina langu ni Kikoyo siyo Chikoyo.

MWENYEKITI: Mheshimiwa Kikoyo.

MHE. DKT. OSCAR I. KIKOYO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa kunipa fursa ya kujibu swali la nyongeza. Wilaya ya Muleba tumejenga zaidi ya shule 30 mpya, lakini walimu wamebaki wale wale. Serikali ina mpango gani mahususi kwa Wilaya ya Muleba kutupatia walimu wa ziada?

Name

Zainab Athuman Katimba

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. ZAINAB A. KATIMBA): Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali inatambua kwamba kumekuwa na shule nyingi mpya ambazo zimejengwa ambazo zina uhitaji mkubwa wa walimu. Tayari Serikali imeanza mikakati mbalimbali ikiwemo kufanya msawazo wa walimu kutoka kwenye shule zile za zamani kuwahamishia kwenye shule hizi mpya. Pia Serikali inatumia njia ya kuajiri walimu ili kufidia upungufu katika maeneo ya shule hizi mpya na hata zile shule za zamani.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, Serikali itaendelea na mikakati hii ili kuhakikisha shule zote zinazojengwa zinaweza kupata walimu ili wanafunzi waweze kupata elimu iliyo bora.

Name

Dr. John Danielson Pallangyo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Arumeru-Mashariki

Primary Question

MHE. YAHYA A. MHATA K.n.y. MHE. HASSAN S. MTENGA aliuliza: - Je, lini Serikali itaongeza Walimu wa Masomo ya Sayansi kwa Shule za Sekondari Mtwara Mjini?

Supplementary Question 4

MHE. DKT. JOHN D. PALLANGYO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana kwa kunipa hii fursa. Shule ya Sekondari Indoombo ina walimu watano tu. Je, ni lini Serikali itapeleka walimu wa kutosha ili kukidhi uwiano unaokubalika kitaifa na kimataifa? (Makofi)

Name

Zainab Athuman Katimba

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. ZAINAB A. KATIMBA): Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nimweleze Mheshimiwa Mbunge kwamba kwa sababu mwaka huu tuna ajira mpya za walimu, kwa hiyo, katika mgao ule tutaangalia kipekee pia kwenye jimbo lake naye aweze kupata mgao wa walimu hao.

Name

Ritta Enespher Kabati

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. YAHYA A. MHATA K.n.y. MHE. HASSAN S. MTENGA aliuliza: - Je, lini Serikali itaongeza Walimu wa Masomo ya Sayansi kwa Shule za Sekondari Mtwara Mjini?

Supplementary Question 5

MHE. DKT. RITTA E. KABATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa Serikali imeanza kupeleka maabara za kompyuta kwenye shule zetu za sekondari nchini: Je, nini mkakati wa Serikali kuhakikisha sasa wale walimu wanajengewa uwezo ili kompyuta hizi ziweze kufanya vizuri zaidi na wanafunzi waweze kupata uelewa wa kutosha?

Name

Zainab Athuman Katimba

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. ZAINAB A. KATIMBA): Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nijibu swali la Mheshimiwa Mbunge, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali itaendelea kuhakikisha kwamba pamoja na ujenzi wa miundombinu na kupatikana kwa vifaa mbalimbali muhimu katika elimu, pia itawajengea uwezo walimu wake ambao wote wanatoa huduma kwa wanafunzi. Kwa hiyo, Serikali itaendelea kuhakikisha hilo.

Name

Bupe Nelson Mwakang'ata

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. YAHYA A. MHATA K.n.y. MHE. HASSAN S. MTENGA aliuliza: - Je, lini Serikali itaongeza Walimu wa Masomo ya Sayansi kwa Shule za Sekondari Mtwara Mjini?

Supplementary Question 6

MHE. BUPE N. MWAKANG’ATA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi. Je, ni lini Serikali itapeleka walimu wa masomo ya sayansi katika Mkoa wa Rukwa hususan Shule ya Sekondari ya Mazwi? (Makofi)

Name

Zainab Athuman Katimba

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. ZAINAB A. KATIMBA): Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Mbunge, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa sababu Serikali katika mwaka huu wa fedha itaajiri walimu 12,000, kwa hiyo katika mgao wa walimu hawa Serikali itaweka jicho la kipaumbele na la kipekee kwenye maeneo yenye upungufu mkubwa ikiwemo katika shule zilizopo katika Mkoa wa Rukwa.