Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 15 Sitting 15 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 192 2024-04-29

Name

Abdi Hija Mkasha

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Micheweni

Primary Question

MHE. ABDI HIJA MKASHA aliuliza: -

Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga Nyumba za Askari wa Jeshi la Uhamiaji Wilaya ya Micheweni?

Name

Daniel Baran Sillo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Babati Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika mwaka wa fedha wa 2023/2024 Serikali imekamilisha taratibu za kufunga mikataba ili kuanza utekelezaji wa mradi wa ujenzi wa nyumba za makazi ya watumishi sanjari na ujenzi wa jengo la Ofisi ya Uhamiaji Wilaya Micheweni. Gharama ya utekelezaji wa mradi huu ni kiasi cha shilingi 2,695,937,724.80, ikijumuisha gharama za mkandarasi kiasi cha shilingi 2,549,937,724.80 na mshauri elekezi kiasi cha shilingi 146,000,000.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na kukamilisha taratibu za ununuzi, tayari Serikali imetoa fedha kiasi cha shilingi 1,250,000,000 ili kuanza utekelezaji wa mradi huu. Aidha, niendelee kumpongeza Mheshimiwa Mbunge kwa ufuatiliaji mzuri wa miradi ya maendeleo kwa wananchi wake, ahsante sana.