Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Abdi Hija Mkasha

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Micheweni

Primary Question

MHE. ABDI HIJA MKASHA aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga Nyumba za Askari wa Jeshi la Uhamiaji Wilaya ya Micheweni?

Supplementary Question 1

MHE. ABDI HIJA MKASHA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa majibu mazuri ya Mheshimiwa Waziri, lakini nina swali moja la nyongeza ambalo lina sehemu (a) na (b) kama ifuatavyo: -

(a) Naomba nitoe taarifa katika hili Bunge kama ndani ya Wilaya yetu ya Micheweni bahati nzuri Ofisi ya Uhamiaji tunayo lakini kubwa ni suala zima la makazi kwa wale askari wetu. Je, ni lini ujenzi huu utaanza?

(b) Je, Waziri yupo tayari kufuatana nami ili twende akajionee uhalisia wa hali ilivyo katika eneo lile? (Makofi)

Name

Constantine John Kanyasu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Geita Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kama nilivyosema kwenye jibu la msingi, ujenzi wa majengo haya ya makazi ya Askari wa Uhamiaji katika Wilaya ya Micheweni itaanza katika mwaka wa fedha 2023/2024 na tayari tumetenga shilingi 1,250,000,000 ili kazi ianze.

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili kuhusu kuongozana na Mheshimiwa Mbunge, nipo tayari kuongozana naye kwenda Micheweni baada ya Bunge la Bajeti, kwa hiyo, asiwe na wasiwasi. ahsante sana, (Makofi)

Name

Sophia Hebron Mwakagenda

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ABDI HIJA MKASHA aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga Nyumba za Askari wa Jeshi la Uhamiaji Wilaya ya Micheweni?

Supplementary Question 2

MHE. SOPHIA H. MWAKAGENDA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Kama shida iliyopo Micheweni Wilaya ya Rungwe pia ina tatizo kama hilo la wafanyakazi wa uhamiaji kutokuwa na makazi ya kudumu ya wafanyakazi wale. Ni lini Serikali itapeleka fedha ili kuwasaidia Askari wale na siyo tu wa Uhamiaji, hata Askari Polisi kwani nyumba zao zimechakaa?

Name

Daniel Baran Sillo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Babati Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nia ya Serikali ni kuhakikisha kwamba Askari wake wote wa Uhamiaji na Askari wote wanakaa makazi yaliyo bora. Nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba jinsi fedha itakavyopatikana, tutatenga fedha kwa ajili ya kujenga nyumba ya makazi kwa ajili ya askari wa Wilaya ya Rungwe, ahsante sana.

Name

Marwa Ryoba Chacha

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Serengeti

Primary Question

MHE. ABDI HIJA MKASHA aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga Nyumba za Askari wa Jeshi la Uhamiaji Wilaya ya Micheweni?

Supplementary Question 3

MHE. MARYAM OMAR SAID: Mheshimiwa Mwenyekiti, kutokana na uchakavu wa nyumba za Polisi zilizopo Finya, Basra maeneo ya Wilaya ya Wete Mkoa wa Kaskazini, ni lini Serikali itafanya ukarabati wa nyumba hizo?

Name

Daniel Baran Sillo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Babati Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Maryam, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kama nilivyosema, nia ya dhati ya Serikali ni kuhakikisha kwamba Askari wake wote; Askari wa Uhamiaji na Askari Polisi, wote wanakaa kwenye makazi ambayo ni bora. Kwa hiyo, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba jinsi fedha zinavyopatikana, tutatenga fedha awamu kwa awamu kuhakikisha Wilaya ya Wete pia inapata ukarabati wa nyumba za Askari wetu.

Name

Omar Issa Kombo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wingwi

Primary Question

MHE. ABDI HIJA MKASHA aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga Nyumba za Askari wa Jeshi la Uhamiaji Wilaya ya Micheweni?

Supplementary Question 4

MHE. OMAR ISSA KOMBO: Mheshimiwa Mwenyekiti, je, ni kazi gani zimefanyika kwenye shilingi 1,250,000,000 ambazo Serikali imepeleka kwenye Wilaya ya Micheweni kama jibu la msingi la Mheshimiwa Naibu Waziri linavyosema?

Name

Daniel Baran Sillo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Babati Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kama nilivyojibu, pengine Mheshimiwa Mbunge hajasikia vizuri, ni kwamba katika mwaka wa fedha huu wa 2023/2024 baada ya kusaini mkataba huu sasa, itaanza kazi ya ujenzi wa nyumba za makazi za askari hawa wa Uhamiaji. Kwa hiyo, kiasi hicho kilichotengwa cha shilingi 1,250,000,000 kitaanza utekelezaji wake mara baada ya kusaini mkataba.

Name

Dr. Angeline Sylvester Lubala Mabula

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Ilemela

Primary Question

MHE. ABDI HIJA MKASHA aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga Nyumba za Askari wa Jeshi la Uhamiaji Wilaya ya Micheweni?

Supplementary Question 5

MHE. DKT. ANGELINE S. L. MABULA: Mheshimiwa Mwenyekiti, swali langu hili sasa naliuliza kwa mara ya tatu na Serikali inaahidi, lakini hakuna kinachofanyika. Naomba nimwulize Mheshimiwa Waziri kwamba, wananchi wamefanya kila juhudi kuweza kujenga boma na limefikia kwenye lintel, lakini tayari kuna maboma sita pale kwa ajili ya Askari: Je, ni lini watakamilisha kazi hii ili kituo kile kianze kufanya kazi na tayari kuna nyumba sita ambazo zina Askari, lakini wanakwenda mbali na kituo hakijaanza kutumika?

Name

Daniel Baran Sillo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Babati Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nawapongeza wananchi wa Jimbo la Ilemela kwa kazi kubwa walioifanya ya ujenzi wa maboma kama alivyosema Mheshimiwa Mbunge. Nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba kazi ambayo wananchi walishaianza, Serikali inaunga mkono na nitapata fursa ya kukaa na Mheshimiwa Mbunge baada ya kipindi hicho niweze kuzungumza naye kuona namna bora ya kumalizia maboma haya ambayo tayari wananchi wameshayajenga.

Name

Minza Simon Mjika

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ABDI HIJA MKASHA aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga Nyumba za Askari wa Jeshi la Uhamiaji Wilaya ya Micheweni?

Supplementary Question 6

MHE. MINZA S. MJIKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, Mkoa wa Simiyu hatuna kabisa nyumba za Askari; Askari Polisi pamoja na Askari wa Uhamiaji. Je, ni lini Serikali itajenga nyumba hizo? (Makofi)

Name

Daniel Baran Sillo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Babati Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nijibu swali la Mheshimiwa Minza, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kama nilivyosema, nia ya Serikali ni kuhakikisha kwamba askari wetu wote wanakaa kwenye makazi bora. Nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba tutaangalia kwenye mwaka huu wa fedha, kama Mkoa wa Simiyu hauna kituo kabisa, basi tuangalie kwenye mwaka wa fedha unaokuja ili kuhakikisha kwamba tunatenga fedha kwa ajili ya ujenzi wa nyumba za Askari Polisi pamoja na Uhamiaji. Nakushukuru sana.