Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 15 Sitting 15 Livestock , Fisheries, Agriculture, Food Security and Cooperatives Wizara ya Kilimo 194 2024-04-29

Name

Mariamu Nassoro Kisangi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MARIAM N. KISANGI aliuliza: -

Je, kuna mpango gani wa kuimarisha kilimo cha Minazi katika Ukanda wa Pwani ya Tanzania?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO alijibu: -
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali kupitia Taasisi ya Utafiti wa Kilimo Tanzania (TARI) imefanya utafiti na kuanzisha aina mpya ya mbegu ya minazi iitwayo East African Tall (EAT) ambayo inastawi katika maeneo ya ukanda wa Pwani na kuvumilia magonjwa. Baada ya kupatikana kwa mbegu hiyo, Serikali katika msimu wa mwaka 2023/2024 imeiwezesha TARI kuzalisha miche 140,000 ambayo itasambazwa kwa wakulima katika Halmashauri za Wilaya za ukanda wa Pwani kuanzia mwezi Oktoba, 2024.

Aidha, jumla ya mbegu za nazi 18,000 zinatarajiwa kusambazwa kwenye vitalu vya Halmashauri za Ruangwa, Mtwara Vijijini, na Muheza. Katika msimu wa 2024/2025 TARI inatarajia kuzalisha miche 200,000 ya aina hiyo ya nazi na kusambaza kwa wakulima.

Mheshimiwa Mwenyekiti, vilevile, Serikali kupitia taasisi zake itaendelea kutoa elimu ya kanuni bora za kilimo cha nazi na teknolojia za uthibiti wa visumbufu vya nazi kwa maafisa ugani na wakulima katika wilaya zote zitakazopatiwa miche mipya kwa ajili ya kufufua mashamba ya nazi.