Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 15 Sitting 15 Health and Social Welfare Wizara ya Afya 198 2024-04-29

Name

Josephine Tabitha Chagulla

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JOSEPHINE T. CHAGULA aliuliza: -

Je, lini Serikali itapeleka Watumishi pamoja na Vifaa Tiba katika Hospitali ya Mkoa wa Geita?

Name

Dr. Godwin Oloyce Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Siha

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA alijibu:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Afya, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Josephine Tabitha Chagula, Mbunge Viti Maalum, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, Hospitali ya Mkoa wa Geita ina jumla ya watumishi 349. Aidha, katika mwaka wa fedha 2023/2024, Serikali imepeleka watumishi 22 wa kada mbalimbali katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Geita. Pia Serikali imepeleka vifaa tiba vyenye thamani ya shilingi bilioni 3.8 kwa ajili ya kuimarisha utoaji wa huduma za afya katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Geita.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuwasilisha.