Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 15 Sitting 45 Health and Social Welfare Wizara ya Afya 586 2024-06-11

Name

Japhet Ngailonga Hasunga (CPA)

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Vwawa

Primary Question

MHE. JAPHET N. HASUNGA aliuliza: -

Je, lini Serikali itajenga Chuo cha Afya Vwawa?

Name

Ummy Ally Mwalimu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Tanga Mjini

Answer

WAZIRI WA AFYA alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Japhet Ngailonga Hasunga, Mbunge wa Vwawa, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, ujenzi wa Chuo cha Afya Vwawa utaanza mwezi Oktoba, 2024 na Serikali imetenga fedha kiasi cha shilingi bilioni 2.9 kwa mwaka wa fedha 2024/2025 kupitia fedha za Mradi wa Mama na Mtoto, kwa ajili ya kujenga jengo la mafunzo mseto (academic complex). Aidha, tayari utaratibu wa kupata eneo umefanyika na kiasi cha shilingi milioni 151 kimetumika kwa ajili ya kulipa fidia ya ardhi kwa wananchi waliopisha eneo hilo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuwasilisha.