Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 15 Sitting 45 Finance and Planning Wizara ya Fedha 590 2024-06-11

Name

Ndaisaba George Ruhoro

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ngara

Primary Question

MHE. NDAISABA G. RUHORO aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa Kituo cha Forodha cha Mugoma?

Name

Dr. Mwigulu Lameck Nchemba Madelu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Iramba Magharibi

Answer

WAZIRI WA FEDHA alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Ndaisaba George Ruhoro, Mbunge wa Ngara, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kabla ya eneo au kituo kuteuliwa kuwa eneo la forodha na kuweza kufunguliwa kama Kituo cha Forodha mahali popote nchini kuna taratibu za kisheria ambazo inabidi zifuatwe. Taratibu hizo ni pamoja na kutangazwa na kuchapishwa kwenye Gazeti la Jumuiya ya Afrika ya Mashariki, kwa mujibu wa Sheria ya Forodha ya Jumuiya ya Afrika ya Mashariki ya mwaka 2004, kifungu namba 11.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tayari tathmini na fidia kwa ajili ya kutoa eneo hilo lilishafanyika na sasa taratibu nyingine za kisheria zinaendelea na baada ya taratibu hizo kukamilika ujenzi utaanza.