Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Ndaisaba George Ruhoro

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ngara

Primary Question

MHE. NDAISABA G. RUHORO aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa Kituo cha Forodha cha Mugoma?

Supplementary Question 1

MHE. NDAISABA G. RUHORO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana, kwanza nimshukuru sana Mheshimiwa Waziri wa Fedha kwa majibu mazuri sana ya Serikali, majibu mazuri yanayotoka kwa Waziri mzuri, tunashukuru sana, nina swali moja la nyongeza. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa Vituo vya Forodha vya Kabanga na Murusagamba vinafungwa saa 1.00 jioni hali ambayo inasababisha adha ya wasafiri wa mabasi kutoendelea na safari zao na magari makubwa kusitisha safari zao kupeleka mzigo nje ya nchi na kufanya nchi ishindwe kutoza kodi na kufanya miji yangu ya mipakani kutokuchangamka kibiashara.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni upi mpango wa Serikali wa kuruhusu vituo hivi vya forodha viweze kufanya kazi saa 24 ili kuweza kuhuwisha biashara ya mpakani?

Name

Dr. Mwigulu Lameck Nchemba Madelu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Iramba Magharibi

Answer

WAZIRI WA FEDHA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nimpongeze Mheshimiwa Mbunge kwa swali lake zuri la nyongeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, niseme tu ametoa kama ushauri kwamba tunapofunga vituo hivi saa nne tunasababisha shughuli zisifanyike kwa muda wote na kwa mantiki hiyo kwa kuwa hiki ni Kituo cha Forodha kinahusisha pande mbili tukifanya masaa 24 upande mmoja bila upande mwingine haitafikia lengo hilo ambalo limekusudiwa.

Kwa hiyo, tumepokea jambo hilo, tutawashirikisha wenzetu wa upande wa pili wa kituo hicho cha forodha ili kuangalia makubaliano ya pamoja ya kufanya kazi kwa saa 24 na tukishakubaliana pande zote mbili basi tutaweza kufanya hivyo ili lengo liweze kutimia. (Makofi)

Name

Aloyce John Kamamba

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Buyungu

Primary Question

MHE. NDAISABA G. RUHORO aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa Kituo cha Forodha cha Mugoma?

Supplementary Question 2

MHE. ALOYCE J. KAMAMBA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali dogo la nyongeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mpaka wa Muhange katika Wilaya ya Kankonko unaunganisha nchi ya Tanzania na Burundi na uwepo wa forodha katika mpaka huo utapelekea Serikali kuweza kuongeza kipato, lakini bahati mbaya eneo hilo mpaka sasa halijajengewa Kituo cha Forodha. Ni lini Kituo cha Forodha kitajengwa katika mpaka wetu wa Muhange? Ahsante. (Makofi)

Name

Dr. Mwigulu Lameck Nchemba Madelu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Iramba Magharibi

Answer

WAZIRI WA FEDHA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru na nimpongeze Mheshimiwa Mbunge kwa kufuatilia sana eneo hilo na Mbunge amefuatilia si tu Kituo cha Forodha bali amekuwa akifuatilia pia barabara inayoelekea eneo hilo. Tulikaa na Waziri wa sekta tumepokea jambo hilo kwa sababu ni barabara na kituo ambacho kinaelekea kwenye makao makuu mapya ya nchi ya Burundi na mimi napanga kufika katika eneo hilo ili kuweza kujionea.

Kwa hiyo, tumepokea tutalifanyia kazi na Mheshimiwa Mbunge tutakupa mrejesho ili uweze kuwaarifu na wananchi wako. (Makofi)