Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 15 Sitting 18 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 229 2024-05-03

Name

Silvestry Fransis Koka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kibaha Mjini

Primary Question

MHE. ISSA J. MTEMVU K.n.y. MHE. SILYVESTRY F. KOKA aliuliza:-

Je, lini Serikali itajenga Daraja la Mto Mpiji ili kuunganisha Kibaha na Kibwegere Wilaya ya Ubungo?

Name

Zainab Athuman Katimba

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. ZAINAB A. KATIMBA) alijibu:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Silyvestry Francis Koka, Mbunge wa Kibaha Mjini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali inatambua umuhimu wa ujenzi wa Daraja la Mto Mpiji linalounganisha Halmashauri ya Mji wa Kibaha na Kibwegere katika Wilaya ya Ubungo. TARURA kwa kushirikiana na Mhandisi Mshauri Smarcon imefanya usanifu wa kina (detailed design) wa daraja hilo lenye urefu wa mita 60. Kazi hiyo imekamilika na inakadiriwa gharama za ujenzi kuwa ni shilingi bilioni tatu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali inaendelea na juhudi za kutafuta fedha kwa ajili ya ujenzi wa daraja hilo, na pindi zitakapopatikana, ujenzi utaanza mara moja.