Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 15 Sitting 18 Works and Transport Wizara ya Ujenzi 235 2024-05-03

Name

Selemani Jumanne Zedi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukene

Primary Question

MHE. SELEMANI J. ZEDI aliuliza: -

Je, lini Serikali itajenga Barabara ya Tabora – Mambali – Bukene hadi Itobo kwa kiwango cha lami?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, ujenzi kwa kiwango cha lami wa Barabara ya Tabora – Mambali – Bukene hadi Itobo kilometa 114, unatekelezwa kwa awamu kulingana na upatikanaji wa fedha. Hadi sasa jumla ya kilometa nane kuanzia Tabora Mjini hadi Nyuzi Round-about zimejengwa kwa kiwango cha lami.

Mheshimiwa Mwenyekiti, aidha, ujenzi wa kilometa moja kuanzia Kijiji cha Uduka kuelekea Kabanga unaendelea na umefikia 60%. Kwa sehemu iliyobaki, Serikali inaendelea kutafuta fedha kwa ajili ya kuendelea na kazi za ujenzi, ahsante. (Makofi)