Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Selemani Jumanne Zedi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukene

Primary Question

MHE. SELEMANI J. ZEDI aliuliza: - Je, lini Serikali itajenga Barabara ya Tabora – Mambali – Bukene hadi Itobo kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 1

MHE. SELEMANI J. ZEDI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kwamba barabara hii inajengwa kwa awamu na awamu, maana yake ni mwaka wa fedha, kwamba ni kidogo kidogo. Swali langu ni kwamba, je, Serikali haioni kwamba kuna umuhimu wa kuongeza idadi ya kilometa kwa hii awamu kwa mwaka wa fedha, kwa sababu tukiendelea na kilometa moja moja kwa kila mwaka wa fedha na barabara hii imebakiza kilometa 104, haoni kwamba itatuchukua miaka 104 kumaliza barabara hii? (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI: Mheshimiwa Mwenyekiti, mpango wa Serikali siyo kuijenga hii barabara kwa awamu kwa kipindi chote, lakini mpango wa Serikali ni kuijenga barabara hii yote kwa kiwango cha lami na ndiyo maana imesanifiwa yote. Kwa kadiri tunavyopata fedha Serikali imeona ni bora tuanze kujenga kwa awamu kadiri fedha zinavyopatikana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tuna uhakika kwamba kadiri tutakavyokuwa tunaendelea, na bajeti itakavyoruhusu, mpango ni kuijenga barabara yote kwa kiwango cha lami kama anavyoomba Mheshimiwa Mbunge, ahsante. (Makofi)

Name

Issaay Zacharia Paulo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbulu Mjini

Primary Question

MHE. SELEMANI J. ZEDI aliuliza: - Je, lini Serikali itajenga Barabara ya Tabora – Mambali – Bukene hadi Itobo kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 2

MHE. ZACHARIA P. ISSAAY: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana. Ni miezi sita sasa Barabara ya Mbulu – Garbabi mkandarasi ameondoka site. Je, ni lini mkandarasi atarudi site kumalizia kazi iliyobaki?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI: Mheshimiwa Mwenyekiti, mkandarasi ambaye anamsema, najua anajenga Mbulu hadi Garbabi, lakini huyu mkandarasi tumesaini naye mkataba wa kuanzia Labay kwenda Haydom na Dareda kwenda Dongobesh na Mheshimiwa Mbunge ni shahidi. Baada ya mvua kukatika, nataka nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba mkandarasi ataendelea na kazi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kilichokuwa kinafanyika ni kujenga makaravati ambayo yalikuwa hayaathiriki na mvua inayoendelea. Kwa hiyo, nataka nimhakikishie kwamba mkandarasi yupo, anaendelea kuzijenga barabara ila tu alikuwa amepunguza kasi.

Name

Rose Vicent Busiga

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SELEMANI J. ZEDI aliuliza: - Je, lini Serikali itajenga Barabara ya Tabora – Mambali – Bukene hadi Itobo kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 3

MHE. ROSE V. BUSIGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, je, ni lini Serikali itakamilisha Barabara ya Geita – Bukoli – Kakola mpaka Kahama kwa kiwango cha lami ili kusaidia kuunganisha Mkoa wa Geita na Shinyanga? (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI: Mheshimiwa Mwenyekiti, barabara aliyoitaja Mheshimiwa Rose ni moja ya barabara ambayo Serikali imeipa kipaumbele kikubwa sana. Ni kweli kwamba Mkoa wa Geita na Mkoa wa Shinyanga ulikuwa haujaunganishwa kwa kiwango cha lami na hii ndiyo ajenda kubwa ya Mkoa wa Geita. Nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba, kuanzia Kahama hadi Ilogi – Kakola, kwa kushirikiana na wenzetu wa bajeti, tayari tumeshasaini mkataba, kwa hiyo, hiyo barabara itajengwa. Tunavyoongea sasa hivi barabara ya kutoka Ilogi – Bukoli – Nyaluyeya hadi Geita, ipo kwenye mpango wa manunuzi ambayo muda wowote itatangazwa ili tuweze kuunganisha Geita na Kahama kwa kiwango cha lami, ahsante. (Makofi)

Name

Prof. Patrick Alois Ndakidemi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Moshi Vijijini

Primary Question

MHE. SELEMANI J. ZEDI aliuliza: - Je, lini Serikali itajenga Barabara ya Tabora – Mambali – Bukene hadi Itobo kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 4

MHE. PROF. PATRICK A. NDAKIDEMI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi. Je, Serikali ina mpango gani wa kurekebisha Barabara ya Chalinze – Segera hadi Himo ambayo imeanza kupoteza ubora wake? (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI: Mheshimiwa Mwenyekiti, barabara aliyoitaja ya Chalinze – Segera hadi Himo ni kati ya barabara ambazo zimejengwa siku nyingi na ni finyu. Sasa hivi tuko tunaifanyia usanifu ili kuweza kuifanyia rehabilitation kwa maana kwanza, ni kuifanya matengenezo makubwa kwa maana ya marekebisho kwa maeneo ambayo ni finyu na pia kule kwenye miinuko kuweza kuipanua na kufanya barabara tatu. Kwa hiyo, huo ndiyo mpango ambao sasa hivi mhandisi mshauri anafanya ili kuibadilisha kabisa hiyo barabara, ahsante. (Makofi)

Name

Aysharose Ndogholi Mattembe

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SELEMANI J. ZEDI aliuliza: - Je, lini Serikali itajenga Barabara ya Tabora – Mambali – Bukene hadi Itobo kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 5

MHE. AYSHAROSE N. MATTEMBE: Mheshimiwa Mwenyekiti, je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa Barabara ya Manyoni – Sanza – Chali hadi Dodoma kwa kiwango cha lami? (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI: Mheshimiwa Mwenyekiti, barabara aliyotaja Mheshimiwa Mbunge sasa hivi tunakamilisha usanifu na baada ya hapo tutaanza kuijenga kwa kiwango cha lami, ahsante. (Makofi)

Name

Esther Nicholus Matiko

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SELEMANI J. ZEDI aliuliza: - Je, lini Serikali itajenga Barabara ya Tabora – Mambali – Bukene hadi Itobo kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 6

MHE. ESTHER N. MATIKO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kwa nini Serikali isitoe kipaumbele kwa barabara za kiusalama ambazo zinapakana na nchi jirani na wilaya mbalimbali za Tanzania, mathalan ile ambayo inapakana na nchi jirani ya Kenya na Wilaya ya Tarime na Rorya kwa mwaka huu wa fedha 2024/2025? (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna vigezo vya kujenga Barabara. Kigezo kimojawapo ni pamoja na barabara za ulinzi. Namhakikishia Mheshimiwa Mbunge kwamba tunapochagua barabara za kuzijenga, ulinzi ni moja ya kigezo kikubwa sana. Kwa hiyo, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba ipo mipango ya kuzijenga hizo Barabara, lakini barabara ziko nyingi, kwa hiyo, tunakwenda kwa awamu kuzijenga hizo barabara, ahsante.

Name

Maimuna Salum Mtanda

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Newala Vijijini

Primary Question

MHE. SELEMANI J. ZEDI aliuliza: - Je, lini Serikali itajenga Barabara ya Tabora – Mambali – Bukene hadi Itobo kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 7

MHE. MAIMUNA S. MTANDA: Mheshimiwa Mwenyekiti, zoezi la ku-mobilize resource katika Barabara ya Mnivata – Newala – Masasi limechukua muda mrefu na barabara haipitiki. Je, ni lini ujenzi rasmi wa lami utaanza ili wananchi wapite vizuri? (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba, kwanza uzuri wa hiyo barabara inafadhiliwa na wenzetu wa African Development Bank na tunafanya ufuatiliaji. Kitu ambacho nawahakikishia Waheshimiwa Wabunge ni kwamba katika kipindi hiki cha mvua na hasa mvua ambayo imezidi, imekuwa zaidi ya wastani, kwa hiyo, kwenye miundombinu ya barabara imekuwa ni ngumu sana kufanya kazi za barabara.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba kama kuna changamoto yoyote ya mobilization kwenye hiyo barabara, tutafuatilia tuone kama kuna changamoto yoyote, ahsante.

Name

Jackson Gedion Kiswaga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalenga

Primary Question

MHE. SELEMANI J. ZEDI aliuliza: - Je, lini Serikali itajenga Barabara ya Tabora – Mambali – Bukene hadi Itobo kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 8

MHE. JACKSON G. KISWAGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, imetokea taharuki kubwa kule Iringa baada ya kusikia Miradi ya REGROW imesimama, wakafikiri kwamba na Mradi wa Ruaha umesimama. Je, Mheshimiwa Waziri atatuambia nini kinaendelea juu ya hii Barabara ya Ruaha? Ahsante. (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba Barabara ya Iringa kwenda Ruaha National Park kilometa 103 haina uhusiano na Program ya REGROW. Hii inafadhiliwa na World Bank na hivi tunavyoongea sasa hivi tuna miradi zaidi ya sita ambayo iko kwenye hiyo package. Sasa hivi tuko kwenye tender evaluation na kilometa zote 103 zinajengwa kutoka Iringa hadi Msembe, Ruaha National Park, ahsante.

Name

Abdallah Dadi Chikota

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nanyamba

Primary Question

MHE. SELEMANI J. ZEDI aliuliza: - Je, lini Serikali itajenga Barabara ya Tabora – Mambali – Bukene hadi Itobo kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 9

MHE. ABDALLAH D. CHIKOTA: Mheshimiwa Mwenyekiti, Barabara ya Kibiti – Lindi imeathiriwa sana na mafuriko yanayoendelea katika maeneo hayo. Je, Serikali ina mpango gani wa matengenezo ya dharura hasa kwenye Daraja la Somanga na Daraja la Mbwemkuru? (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kwamba moja ya barabara ambazo zimeathirika sana ni barabara ya Kusini na ndiyo barabara kuu. Tunamshukuru Mungu tu kwamba mpaka sasa hivi walau watu wanaweza kupita, lakini tumeshaainisha maeneo yote ambayo yamepata changamoto kubwa na hasa kutokana na hii changamoto ya mvua.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba bado maji yanaendelea kupita, kwa hiyo, baada ya kukauka Serikali imejipanga kuhakikisha kwamba tunarejesha mawasiliano. Hiyo ndiyo itakuwa kazi ya kwanza kurejesha mawasiliano na kuimarisha barabara zile zilizoharibika ili ziweze kurudi katika hali yake ya kawaida ikiwa ni pamoja na barabara muhimu sana ya kwenda Kusini aliyoitaja Mheshimiwa Chikota, ahsante. (Makofi)