Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
---|---|---|---|---|---|---|
2020-2025 | Session 15 | Sitting 34 | Youth, Disabled, Labor and Employment | Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Ajira, Vijana na Wenye Ulemavu | 439 | 2024-05-27 |
Name
Khadija Shaaban Taya
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Primary Question
MHE. KHADIJA S. TAYA aliuliza:-
Je, ni lini Serikali itahakikisha kunakuwa na maeneo maalum ya Watu wenye Ualbino kwenye mikutano ya hadhara ili wasikae juani?
Name
Ummy Hamisi Nderiananga
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Answer
NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, SERA, BUNGE NA URATIBU (MHE. UMMY H. NDERIANANGA) alijibu:-
Mheshimiwa Spika, Sera ya Taifa ya Maendeleo na Huduma kwa Watu Wenye Ulemavu ya 2004, kupitia matamko yake namba 3, Kifungu cha 11 - Uondoaji Vikwazo vya Ufikivu, 3:1-Matunzo kwa Watu wenye Ulemavu, 3(13) kuhusu Marekebisho na 3(14) - Mchangamano, imeonesha namna ambayo watu wenye ulemavu wakiwemo wenye Ualbino wanavyostahili kushiriki na kushirikishwa katika shughuli za kijamii na kisiasa. Aidha, Sheria ya Watu wenye Ulemavu, Sura Na.183, Sehemu ya Nne, Kifungu cha 15(1) na Sehemu ya Tisa, Kifungu cha 51 zinabainisha juu ya ushiriki wa watu wenye ulemavu katika shughuli za kijamii na kisiasa.
Mheshimiwa Spika, kwa kuzingatia nyaraka hizi muhimu, Serikali inatoa wito kwa viongozi wote wa Serikali na Taasisi zake pamoja na Taasisi na wadau wa huduma za kijamii kuhakikisha kuwa wakati wa utoaji wa huduma, suala la ufikivu na usalama kwa watu wenye Ualbino linazingatiwa. Aidha, Serikali inaendelea kutoa wito kwa watu wenye Ualbino kutambua mahitaji na haki zao kiafya na kujiepusha na mazingira yanayoweza kuhatarisha afya zao. Ahsante.
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved