Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Name
Khadija Shaaban Taya
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Primary Question
MHE. KHADIJA S. TAYA aliuliza:- Je, ni lini Serikali itahakikisha kunakuwa na maeneo maalum ya Watu wenye Ualbino kwenye mikutano ya hadhara ili wasikae juani?
Supplementary Question 1
MHE. KHADIJA S. TAYA: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa majibu mazuri ya Serikali, pamoja na majibu hayo nina maswali mawili ya nyongeza.
Swali la kwanza, kwa kuwa tatizo hilo bado lipo na linajitokeza. Je, ni kwa kiasi gani watendaji wanaufahamu wa sera hii ambayo Mheshimiwa Naibu Waziri umeisema?
Mheshimiwa Spika, swali langu la pili; je, sasa Serikali haioni haja ya kutoa mwongozo tena mara nyingine kwa watendaji wanaohusika na masuala ya sherehe za Serikali?
Name
Ummy Hamisi Nderiananga
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Answer
NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, SERA, BUNGE NA URATIBU (MHE. UMMY H. NDERIANANGA): Mheshimiwa Spika, naomba nimshukuru Mheshimiwa Keysha, kama nilivyojibu jibu la msingi tuna sera na sheria. Nitoe rai kwa wale wanaoandaa shughuli za Serikali na sisi Ofisi ya Waziri Mkuu chini ya Waziri wetu Mheshimiwa Jenista, tumekuwa tukifanya jambo hili kwa pamoja. Maadhimisho mbalimbali ya sherehe tuna kitengo cha sherehe waendelee kuweka nafasi hizi za watu wenye Ualbino na watu wengine kwa sababu tunaweka masuala ya tenti kuweka vizuri ili waweze kukaa. Tuna mkakati gani? Tunaendelea kushirikiana na Chama cha Watu Wenye Ualbino Tanzania (TAS) pamoja na wadau wengine wanaofanya kazi kwenye eneo la watu wenye ulemavu kujengea elewa jamii ili kufahamu haki za watu wenye ulemavu na sera.
Mheshimiwa Spika, pia tuko kwenye marekebisho ya Sera ya Taifa ya Watu Wenye Ulemavu ambayo pia nayo inagusa kundi la watu wenye Ualbino. Kwa hiyo nimtoe mashaka Mheshimiwa Khadija Shaaban Taya maarufu kama Keysha kwamba mambo yanaenda vizuri Serikali ya Awamu ya Sita, Mheshimiwa Rais, Daktari Samia tunaendelea kuwajali watu wenye ulemavu na watu wenye Ualbino. Ahsante. (Makofi)
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved