Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
---|---|---|---|---|---|---|
2020-2025 | Session 18 | Sitting 1 | Information, Communication and Information Technology | Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari | 10 | 2025-01-28 |
Name
Bahati Keneth Ndingo
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Mbarali
Primary Question
MHE. BAHATI K. NDINGO aliuliza:-
Je, lini Serikali itafanya zoezi la Anwani za Makazi katika baadhi ya maeneo ya Rujewa, Imalilo, Songwe na Mwatenga ambayo bado hayajafanyika?
Name
Maryprisca Winfred Mahundi
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Answer
NAIBU WAZIRI WA MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI alijibu: -
Mheshimiwa Spika, itakumbukwa kwamba utekelezaji wa Mfumo wa Anwani za Makazi ulifanyika Februari hadi Mei 2022 kwa njia ya operesheni. Hatua hii ilikuwa ni utekelezaji wa maelekezo ya Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, aliyoyatoa tarehe 8 Februari, 2022. Kupitia Operesheni ya Anwani za Makazi Mfumo wa Anwani za Makazi ulitekelezwa nchi nzima.
Mheshimiwa Spika, utekelezaji wa Mfumo wa Anwani za Makazi ni endelevu kwa sababu ya mabadiliko ya makazi, wakazi na huduma. Ili kuweka mazingira endelevu ya utekelezaji kila mkoa na halmashauri ina mratibu/waratibu wa kusimamia utekelezaji, uendelezaji na matumizi ya mfumo.
Mheshimiwa Spika, aidha, Wizara kwa kushirikiana na Ofisi ya Rais, TAMISEMI itatuma wataalam wake katika Halmashauri ya Mbarali kufanya ufuatiliaji, ikiwa ni pamoja na kutembelea maeneo yaliyoainishwa na Mheshimiwa Mbunge ili kubaini mapungufu kwa ajili ya kuchukua hatua.
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved