Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
---|---|---|---|---|---|---|
2000-2005 | Session 12 | Sitting 6 | Water and Irrigation | Wizara ya Maji | 97 | 2025-02-04 |
Name
Anatropia Lwehikila Theonest
Sex
Female
Party
CHADEMA
Constituent
Special Seats
Primary Question
MHE. ANATROPIA L. THEONEST aliuliza: -
Je, lini miradi ya maji Wilayani Kyerwa itakamilika ili Wananchi wapate huduma ya maji?
Name
Jumaa Hamidu Aweso
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Pangani
Answer
WAZIRI WA MAJI alijibu: -
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Anatropia Theonest, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -
Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali inaendelea na utekelezaji wa miradi sita ya maji katika Wilaya ya Kyerwa ambayo ni Runyinya - Chanya, Kikukuru, Kimuli – Rwanyango - Chakalisa, Kaisho - Isingiro, Nyamyaga - Nayakatera na Mabira. Hadi kufikia mwezi Januari, 2025, Serikali imekamilisha utekelezaji wa miradi miwili ya Nyamyaga – Nayakatera na Mibira ambayo inahudumia wananchi 26,218 waishio kwenye Kata za Bugomora na Mabira. Ujenzi wa miradi iliyobaki upo katika hatua za mwisho za utekelezaji na unatarajiwa kukamilika ifikapo mwezi Juni, 2025.
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved