Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
---|---|---|---|---|---|---|
2020-2025 | Session 18 | Sitting 8 | Regional Administration and Local Government Authorities | Ofisi ya Rais TAMISEMI. | 128 | 2025-02-06 |
Name
Khadija Shaaban Taya
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Primary Question
MHE. KHADIJA S. TAYA aliuliza:-
Je, Wakuu wa Wilaya wametekeleza kwa kiasi gani agizo la Waziri Mkuu la kutenga ofisi za watu wenye ulemavu katika ofisi zao?
Name
Dr. Festo John Dugange
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Wanging'ombe
Answer
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE) alijibu:-
Mheshimiwa Spika, katika kutekeleza maagizo ya Mheshimiwa Waziri Mkuu aliyoyatoa wakati wa ufunguzi wa Kongamano la Watu Wenye Ulemavu, Mkoani Dar es Salaam Agosti, 2023, mikoa kwa kushirikiana na halmashauri imeendelea kuratibu upatikanaji wa Ofisi za Vyama vya Watu Wenye Ulemavu.
Mheshimiwa Spika, kufikia Januari, 2025 Mikoa 26 na Wilaya 73 zimetenga ofisi za Vyama vya Watu Wenye Ulemavu katika majengo ya Halmashauri, Ofisi za Wakuu wa Wilaya na Ofisi za Kata.
Mheshimiwa Spika, Serikali inaendelea na jitihada za kuhakikisha ofisi za Vyama vya Watu Wenye Ulemavu zinapatikana katika wilaya zote nchini. Ahsante.
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved