Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
---|---|---|---|---|---|---|
2020-2025 | Session 18 | Sitting 3 | Regional Administration and Local Government Authorities | Ofisi ya Rais TAMISEMI. | 41 | 2025-01-30 |
Name
Mwantumu Mzamili Zodo
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Primary Question
MHE. MWANTUMU M. ZODO aliuliza: -
Je, lini Serikali itaweka mkakati madhubuti wa upatikanaji wa maji ya uhakika kwenye Shule za Msingi na Sekondari nchini?
Name
Zainab Athuman Katimba
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Answer
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. ZAINAB A. KATIMBA) alijibu: -
Mheshimiwa Spika, Serikali inatekeleza mikakati mbalimbali kuhakikisha upatikanaji wa maji ya uhakika kwenye shule za msingi na sekondari nchini. Mikakati hiyo ni pamoja na kutoa fedha kwa baadhi ya shule kwa ajili ya kuchimba visima virefu na vifupi, kutoa fedha kwa ajili ya kujenga miundombinu ya kuvuna maji ya mvua na kununua matanki makubwa kwa ajili ya kuhifadhia maji na kutoa elimu ya namna ya kuhifadhi vyanzo vya maji vilivyopo katika maeneo yao ili maji hayo yasaidie kutumiwa na shule zilizopo jirani na vyanzo hivyo.
Mheshiwa Spika, Ofisi ya Rais, TAMISEMI itaendelea kushirikiana na Wizara ya Maji kuhakikisha kuwa shule za msingi na sekondari zinapata vyanzo vya maji vya uhakika.
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved