Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
---|---|---|---|---|---|---|
2020-2025 | Session 18 | Sitting 3 | Regional Administration and Local Government Authorities | Ofisi ya Rais TAMISEMI. | 42 | 2025-01-30 |
Name
Jackson Gedion Kiswaga
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Kalenga
Primary Question
MHE. JACKSON G. KISWAGA aliuliza: -
Je, Serikali ina mpango gani wa kuwasikiliza Wananchi wa Kitongoji cha Bandabichi, Kijiji cha Ifunda, ambao walihamishiwa katika Kijiji cha Kivalali bila ridhaa?
Name
Zainab Athuman Katimba
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Answer
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. ZAINAB A. KATIMBA) alijibu: -
Mheshimiwa Spika, mabadiliko ya mipaka ya maeneo ya utawala yamekuwa yakifanyika kwa kuzingatia Mwongozo wa Uanzishaji wa Maeneo ya Utawala katika Mamlaka za Serikali za Mitaa wa Mwaka 2014. Serikali kupitia barua yenye Kumb. Na. CFA.89/141/01/"C"/19 ya tarehe 16 Januari, 2024 ilipokea ombi la kuhamishwa Vitongoji vya Kibaoni B, Bandabichi na Ifunda Sekondari vilivyopo Kijiji cha Bandabichi, Kata ya Ifunda, vihamie Kijiji cha Ifunda. Aidha, Ofisi ya Rais, TAMISEMI imeshafanyia kazi maombi hayo na kutangazwa kwenye Gazeti la Serikali Na. 796 la Agosti, 2024.
Mheshimiwa Spika, ikiwa kusudio la sasa ni kukirejesha Kitongoji cha Bandabichi katika Kijiji cha Bandabichi kilipokuwa awali, naishauri halmashauri kufuata utaratibu ulioainishwa kwenye Sheria ya Uanzishwaji wa Maeneo ya Kiutawala kwa ajili ya kuendelea na utekelezaji.
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved