Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
---|---|---|---|---|---|---|
2020-2025 | Session 18 | Sitting 3 | Regional Administration and Local Government Authorities | Ofisi ya Rais TAMISEMI. | 43 | 2025-01-30 |
Name
Issa Ally Mchungahela
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Lulindi
Primary Question
MHE. ISSA A. MCHUNGAHELA aliuliza: -
Je, kwa nini ajira za muda kama za kuandikisha wapiga kura zisitolewe kwa watu wasio na ajira badala ya kuwapa watu walioajiriwa?
Name
Zainab Athuman Katimba
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Answer
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. ZAINAB A. KATIMBA) alijibu: -
Mheshimiwa Spika, ajira za muda za uandikishaji wa wapiga kura zipo kwa mujibu wa Kanuni ya 9 (2) ya Kanuni za Uchaguzi za Mwaka 2024. Tangazo la Serikali Na. 572 na Kanuni ya 10 (2) ya Kanuni za Uchaguzi wa Serikali za Mitaa za Mwaka 2024, zinaelekeza Msimamizi wa Uchaguzi kufanya uteuzi wa watumishi wa umma watakaoandikisha na kuandaa orodha ya wapiga kura.
Mheshimiwa Spika, hata hivyo, wakati wa Uchaguzi wa Serikali za Mitaa wa Mwaka 2024, shughuli nyingine za ukarani (usaidizi katika vituo) zilitolewa pia, kwa watu wasio na ajira katika vituo vipatavyo 80,584.
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved