Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
---|---|---|---|---|---|---|
2020-2025 | Session 18 | Sitting 3 | Planning and Investment | Ofisi ya Rais: Mipango na Uwekezaji | 45 | 2025-01-30 |
Name
Dr. Pius Stephen Chaya
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Manyoni Mashariki
Primary Question
MHE. DKT. PIUS S. CHAYA aliuliza: -
Je, lini Serikali itaunda Mamlaka ya Usimamizi wa Uwekezaji wa Umma ili kuimarisha usimamizi wa uwekezaji ndani ya Serikali?
Name
Stanslaus Haroon Nyongo
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Maswa Mashariki
Answer
NAIBU WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, MIPANGO NA UWEKEZAJI alijibu: -
Mheshimiwa Spika, uundwaji wa Mamlaka ya Usimamizi wa Uwekezaji wa Umma unasubiri kupitishwa kwa Sheria ya Mamlaka ya Uwekezaji wa Umma, ambapo Muswada wa sheria hiyo, umesomwa kwa mara ya kwanza mwezi Novemba, 2023 na kuelekezwa kwenye Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Uwekezaji wa Mitaji ya Umma (PIC) kwa ajili ya uchambuzi. Mara baada ya Kamati kukamilisha kazi hiyo, Muswada huo utaletwa hapa Bungeni kwa ajili ya hatua nyingine zinazofuata za utungwaji wa sheria.
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved