Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
---|---|---|---|---|---|---|
2000-2005 | Session 12 | Sitting 3 | Energy and Minerals | Wizara ya Nishati | 46 | 2025-01-30 |
Name
Selemani Jumanne Zedi
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Bukene
Primary Question
MHE. SELEMANI J. ZEDI aliuliza: -
Je, lini vijiji vya Bukene na Itobo vitaunganishiwa umeme kwa gharama ya shilingi 27,000 kama vijiji vingine?
Name
Judith Salvio Kapinga
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Answer
NAIBU WAZIRI WA NISHATI alijibu: -
Mheshimiwa Spika, kutokana na hali halisi ilivyo nchini, kuna maeneo ya vijiji na vijiji miji. Serikali inaendelea kuwahakikishia wananchi kwamba maeneo yote ya vijiji yataendelea kuunganishwa umeme kwa gharama ya shilingi 27,000. Maeneo ya Bukene na Itobo ni vijiji miji, hivyo, gharama ya kuunganisha umeme ni shilingi 320,960. Serikali inaendelea kuangalia kama kuna uwezekano wa kufanya maboresho kutokana na tathmini iliyofanyika, ahsante.
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved