Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
---|---|---|---|---|---|---|
2020-2025 | Session 18 | Sitting 3 | Justice and Constitutional Affairs | Wizara ya Katiba na Sheria | 47 | 2025-01-30 |
Name
Rose Cyprian Tweve
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Primary Question
MHE. ROSE C. TWEVE aliuliza: -
Je, lini Serikali itaweka adhabu kubwa zaidi kwa wanaokutwa na hatia ya unyanyasaji?
Name
Geophrey Mizengo Pinda
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Kavuu
Answer
NAIBU WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI K.n.y. WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA alijibu: -
Mheshimiwa Spika, makosa mengi ya unyanyasaji yamebainishwa katika Sehemu ya 15 ya Sheria ya Kanuni ya Adhabu, Sura ya 16, ambapo kuna makosa ya kubaka, kulawiti, kuzini na maalimu, shambulio la aibu, kunajisi punguani na kadhalika ambayo yana adhabu tofauti kulingana na aina na ukubwa wa kosa. Adhabu ya juu kwa makosa ya aina hii ni kifungo cha maisha jela na adhabu ya chini kabisa katika makosa haya ni kifungo cha miaka mitano kwa kosa la shambulio la aibu.
Mheshimiwa Spika, adhabu hizi zimewekwa kwa kuzingatia uzito wa kosa lililotendwa, hivyo Serikali bado inaamini adhabu hizo zinajitosheleza kuwa fundisho kwa wakosaji wa makosa haya.
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved