Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
---|---|---|---|---|---|---|
2020-2025 | Session 18 | Sitting 3 | Water and Irrigation | Wizara ya Maji | 48 | 2025-01-30 |
Name
Bupe Nelson Mwakang'ata
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Primary Question
MHE. DKT. CHRISTINE G. ISHENGOMA K.n.y. MHE. BUPE N. MWAKANG’ATA aliuliza: -
Je, lini Serikali itamaliza Mradi wa Maji Isale Wilayani Nkasi?
Name
Kundo Andrea Mathew
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Bariadi
Answer
NAIBU WAZIRI WA MAJI alijibu: -
Mheshimiwa Spika, Serikali inaendelea na utekelezaji wa mradi wa maji Isale unaolenga kunufaisha vijiji sita vya Isale, Msilihofu, Ntuchi, Ifundwa, Kitosi na Nkata. Kazi zinazotekelezwa katika mradi huo ni pamoja na ujenzi wa chanzo cha maji (intake), ulazaji wa mabomba umbali wa kilometa 70.22, ujenzi wa matanki sita yenye jumla ya ujazo wa lita 420,000 na ujenzi wa vituo 75 vya kuchotea maji. Utekelezaji wa mradi huo umefikia wastani wa 78% na umeanza kutoa huduma ya maji kwenye vijiji viwili vya Nkata na Kitosi. Mradi huo unatarajiwa kukamilika mwezi Juni, 2025 na kunufaisha wananchi 20,113 wa vijiji hivyo. (Makofi)
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved