Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
---|---|---|---|---|---|---|
2020-2025 | Session 18 | Sitting 3 | Water and Irrigation | Wizara ya Maji | 49 | 2025-01-30 |
Name
Noah Lemburis Saputi Mollel
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Arumeru-Magharibi
Primary Question
MHE. NOAH L. S. MOLLEL aliuliza: -
Je, lini Serikali itakamilisha mradi wa maji wa Kata ya Kimnyaki, Tarakwa, Kiranyi na Siwandeti ambayo ni ahadi ya Waziri wa Maji?
Name
Kundo Andrea Mathew
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Bariadi
Answer
NAIBU WAZIRI WA MAJI alijibu: -
Mheshimiwa Spika, Serikali inaendelea na utekelezaji wa Mradi wa Maji wa Kata ya Kimnyaki, Tarakwa, Kiranyi na Siwandeti Wilayani Arumeru. Kazi zinazofanyika katika mradi huo ni ujenzi wa tanki la kukusanyia maji (sump well) lenye ujazo wa lita 50,000, ununuzi na ufungaji wa pampu mbili zenye uwezo wa kuzalisha maji lita 1,560,000 kwa siku, ulazaji wa mabomba ya usambazaji umbali wa kilometa 67, pamoja na ujenzi wa vituo 70 vya kuchotea maji.
Mheshimiwa Spika, utekelezaji wa mradi umefikia wastani wa 80% na umeanza kutoa huduma katika maeneo ya Olmringaringa na Kimnyaki kupitia vituo 13 vilivyojengwa. Mradi unatarajiwa kukamilika mwezi Juni, 2025 na utanufaisha wananchi wapatao 57,541 waishio maeneo hayo. Ahsante.
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved