Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
---|---|---|---|---|---|---|
2000-2005 | Session 12 | Sitting 9 | Regional Administration and Local Government Authorities | Ofisi ya Rais TAMISEMI. | 138 | 2025-02-07 |
Name
Mwita Mwikwabe Waitara
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Tarime Vijijini
Primary Question
MHE. MWITA M. WAITARA aliuliza: -
Je, lini Serikali itapeleka Gari la Mkuu wa Wilaya ya Tarime?
Name
Dr. Festo John Dugange
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Wanging'ombe
Answer
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE) alijibu: -
Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2024/2025, Serikali ilitenga na kuidhinisha shilingi Milioni 504.7 kwa ajili ya ununuzi wa magari mawili aina ya Toyota Land Cruiser Prado kwa ajili ya Wakuu wa Wilaya ya Tarime na Musoma.
Mheshimiwa Spika, taratibu za malipo kwa ajili ya ununuzi wa magari hayo zimefanyika Januari, 2025 kupitia kwa Wakala wa Huduma ya Ununuzi Serikalini (GPSA) na hatua za manunuzi zinaendelea.
Mheshimiwa Spika, mpango wa Serikali ni kuyapata magari hayo likiwemo gari la Mkuu wa Wilaya ya Tarime ndani ya mwaka huu wa fedha, ahsante.
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved