Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
---|---|---|---|---|---|---|
2020-2025 | Session 18 | Sitting 9 | Regional Administration and Local Government Authorities | Ofisi ya Rais TAMISEMI. | 141 | 2025-02-07 |
Name
Justin Lazaro Nyamoga
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Kilolo
Primary Question
MHE. JUSTIN L. NYAMOGA aliuliza: -
Je, lini Serikali itakamilisha ujenzi wa miundombinu ya Shule Shikizi za Msingi zilizoanzishwa kwa nguvu za Wananchi – Kilolo?
Name
Zainab Athuman Katimba
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Answer
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (ZAINAB A. KATIMBA) alijibu: -
Mheshimiwa Spika, Halmashauri ya Wilaya ya Kilolo ina jumla vituo shikizi 18 vilivyoanzishwa kwa nguvu za wananchi ambavyo ni Kichangani, Msombwe, Mlewela, Madizini, Igingilanyi, Mabondwa, Kware, Mapangali, Muungano, Lugolofu, Ilangamoto, Ubandusi, Barabarambili, Kidumka, Lulindi, Kitemela, Kisanzala na Masimike.
Mheshimiwa Spika, kwa mwaka 2024/2025, Serikali ilipeleka shilingi milioni 701 kwa ajili ya ujenzi wa shule mbili mpya za mkondo mmoja katika vituo shikizi vya Kichangani na Msombwe. Ujenzi wa shule hizi upo hatua ya ukamilishaji.
Mheshimiwa Spika, Serikali itaendelea kutenga fedha za kukamilisha ujenzi wa miundombinu katika vituo shikizi vilivyoanzishwa kwa nguvu za wananchi kadri ya upatikanaji wa fedha.
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved