Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
---|---|---|---|---|---|---|
2020-2025 | Session 18 | Sitting 9 | Energy and Minerals | Wizara ya Nishati | 142 | 2025-02-07 |
Name
Yahya Ally Mhata
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Nanyumbu
Primary Question
MHE. ALLY Y. MHATA aliuliza: -
Je, lini Serikali itashusha bei ya kuunganisha umeme katika Kata za Mangaka na Kilimanihewa kama maombi yalivyowasilishwa Wizarani?
Name
Judith Salvio Kapinga
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Answer
NAIBU WAZIRI WA NISHATI alijibu: -
Mheshimiwa Spika, kutokana na hali halisi ilivyo nchini, kuna maeneo ya vijiji na vijiji miji ambapo maeneo ya vijiji yanaunganishwa umeme kwa gharama ya shilingi 27,000/= na maeneo yenye sura ya vijiji miji, yanaunganishwa kwa gharama ya shilingi 320,960/=. Kwa maeneo ya Kata ya Mangaka na Kilimahewa yenye sura ya vijiji miji yanaunganishiwa umeme kwa gharama ya shilingi 320,960/=. Serikali inaendelea kuangalia kama kuna uwezekano wa kufanya maboresho kutokana na tathmini iliyofanyika, ahsante.
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved