Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
---|---|---|---|---|---|---|
2020-2025 | Session 18 | Sitting 9 | Energy and Minerals | Wizara ya Madini | 143 | 2025-02-07 |
Name
Tumaini Bryceson Magessa
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Busanda
Primary Question
MHE. TUMAINI B. MAGESSA aliuliza: -
Je, lini Serikali itapitia upya tozo zilizopo kwenye mnyororo wa uchimbaji na uchenjuaji wa dhahabu zinazowaelemea wachimbaji wadogo?
Name
Anthony Peter Mavunde
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Dodoma mjini
Answer
WAZIRI WA MADINI alijibu: -
Mheshimiwa Spika, Wizara kupitia Mkakati wa Kuboresha Mazingira ya Biashara Nchini (MKUMBI) imefanya utafiti wa tozo 66 zinazotozwa na halmashauri katika shughuli za madini ikiwemo madini ya dhahabu. Tozo zilizobainika katika shughuli za uchimbaji na uchenjuaji wa dhahabu ni pamoja na ushuru wa karasha, ada ya ukaguzi, VAT leaching, Mialo, ushuru wa kusafirisha miamba ya madini na visusi (mabaki ya miamba baada ya kuchenjuliwa).
Mheshimiwa Spika, katika kutatua changamoto hizi Wizara iliitisha kikao mwezi Agosti, 2024 Mkoani Singida ambacho kilishirikisha Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa; Wizara ya Fedha; Tume ya Madini; STAMICO; Halmashauri za Wilaya za Ikungi, Chunya, Kahama, Msalala, Meatu, Shinyanga, Mtama na Lindi; FEMATA; na TAWOMA. Rasimu ya mapendekezo ya maboresho tayari imeshaandaliwa na ipo katika hatua ya kufanyiwa mapitio na tathmini, ambapo matokeo ya tathmini hiyo yatatusaidia katika kupanga tozo rafiki kwa wachimbaji wadogo.
Mheshimiwa Spika, kutokana na changamoto za kikodi nchini, Mheshimiwa Rais ameunda Tume ya Maboresho ya Kodi ili ifanye tathmini ya mfumo wa kodi na kuleta mapendekezo ya namna ya kuboresha mfumo wa kodi. Ni imani yetu kuwa maboresho hayo yataangazia changamoto za kikodi zinazoikabili Sekta ya Madini.
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved