Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
---|---|---|---|---|---|---|
2020-2025 | Session 18 | Sitting 9 | Justice and Constitutional Affairs | Wizara ya Katiba na Sheria | 144 | 2025-02-07 |
Name
Stella Simon Fiyao
Sex
Female
Party
CHADEMA
Constituent
Special Seats
Primary Question
MHE. STELLA S. FIYAO aliuliza: -
Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga Mahakama ya Wilaya Momba?
Name
Sagini Jumanne Abdallah
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Butiama
Answer
NAIBU WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA alijibu: -
Mheshimiwa Spika, Serikali kwa kushirikiana na Mahakama ya Tanzania, imeendelea kutekeleza mpango wa ujenzi na ukarabati wa Mahakama kwa kuimarisha majengo ya Mahakama katika ngazi mbalimbali, ikiwa ni pamoja na kujenga majengo mapya na kukarabati yaliyopo.
Mheshimiwa Spika, katika Mpango huo, ujenzi wa jengo la Mahakama ya Wilaya ya Momba utatekelezwa kwa bajeti ya mwaka 2024/2025. Kwa sasa mradi huo upo hatua ya mwisho ya manunuzi ya kupata mkandarasi wa ujenzi. Hivyo, ujenzi unatarajiwa kuanza ndani ya mwezi Februari, 2025, ahsante.
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved