Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
---|---|---|---|---|---|---|
2020-2025 | Session 18 | Sitting 9 | Industries and Trade | Wizara ya Viwanda na Biashara | 145 | 2025-02-07 |
Name
Eric James Shigongo
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Buchosa
Primary Question
MHE. OLIVER D. SEMUGURUKA K.n.y. MHE. ERIC J. SHIGONGO aliuliza: -
Je, lini Serikali itafufua kiwanda cha kuchambua Pamba cha Nyakarilo, Buchosa?
Name
Exaud Silaoneka Kigahe
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Mufindi Kaskazini
Answer
NAIBU WAZIRI WA VIWANDA NA BIASHARA alijibu:-
Mheshimiwa Spika, Serikali kupitia Bodi ya Pamba (TCB) mwaka 2020 ilifanya tathmini juu ya hali ya viwanda vya kuchambua pamba nchini. Tathmini hiyo imewezesha ukarabati wa baadhi ya viwanda hivyo. Viwanda vilivyokuwa vinahitaji ukarabati mkubwa ni pamoja na kiwanda cha kuchambua pamba cha Nyakarilo.
Mheshimiwa Spika, Serikali kupitia Benki ya Kilimo ilianzisha utaratibu wa dirisha maalum la kuvikopesha viwanda husika. Baadhi ya viwanda vilivyopata mikopo, kukamilisha ukarabati na kuanza kufanya kazi ni pamoja na Chato Cooperative Union, Mbogwe Cooperative Union, Kahama Cooperative Union na Sola. Kwa kutumia utaratibu huo, Serikali itahakikisha pia kiwanda cha Nyakarilo kinakarabatiwa ili kuongeza tija katika mnyororo mzima wa sekta ya pamba. Nakushukuru.
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved