Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
---|---|---|---|---|---|---|
2020-2025 | Session 18 | Sitting 9 | Lands, Housing and Human Settlement Development | Wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi | 146 | 2025-02-07 |
Name
Asia Abdulkarim Halamga
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Primary Question
MHE. ASIA A. HALAMGA aliuliza:-
Je, lini Wananchi waliolipia upimaji watapewa Hati za umiliki wa Ardhi - Hanang?
Name
Geophrey Mizengo Pinda
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Kavuu
Answer
NAIBU WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI alijibu:-
Mheshimiwa Spika, jumla ya mashamba 5,506 yamepimwa katika Kata za Gitting, Masakta, Ishponga, Dirma, Balangdalalu, Gehandu na Mogitu. Aidha, jumla ya viwanja 11,440 vimepimwa katika Halmashauri ya Wilaya ya Hanang katika kata za Ganana, Endasiwold, Nangwa, Bassotu, Dumbeta, Katesh na Balangdalalu. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, baada ya upimaji kukamilika, wananchi wameandaliwa nyaraka za umiliki wa ardhi zao ambapo jumla ya Hati za Hakimiliki za Kimila 1,360 zimeandaliwa na kutolewa kwa wananchi wa kata za Gitting (150), Masakta (210) na Ishponga (1,000). Aidha, jumla ya Hatimiliki 1,505 zimeandaliwa na kutolewa katika Kata za Gitting (355), Masakta (205) na Ishponga (950).
Mheshimiwa Spika, zoezi la kuandaa Hatimiliki na Hati za Hakimiliki za Kimila bado linaendelea kutegemeana na ukamilishwaji wa masharti ya umiliki wa ardhi kwa wananchi husika. Aidha, Serikali inaendelea kushughulikia changamoto na malalamiko ya wananchi yanayoendelea kujitokeza wakati wa zoezi la umilikishwaji ardhi kwa mujibu wa sheria, kanuni na taratibu.
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved