Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
---|---|---|---|---|---|---|
2020-2025 | Session 18 | Sitting 9 | Home Affairs | Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi | 147 | 2025-02-07 |
Name
Emmanuel Peter Cherehani
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Ushetu
Primary Question
MHE. EMMANUEL P. CHEREHANI aliuliza:-
Je, Serikali ina mpango gani wa kupeleka gari Ofisi ya Uhamiaji Wilaya ya Kahama ili kuboresha utendaji kazi?
Name
Daniel Baran Sillo
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Babati Vijijini
Answer
NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu:-
Mheshimiwa Spika, Ofisi ya Uhamiaji Wilaya ya Kahama kwa sasa ina gari moja yenye namba za usajili STL 1022 aina ya Ford Ranger pick - up double cabin ambayo ni chakavu. Aidha, Serikali kupitia Idara ya Uhamiaji imetenga kiasi cha fedha shilingi 3,259,987,000 katika mwaka wa fedha 2024/2025 kwa ajili ya ununuzi wa magari 18 kwa ajili ya kuimarisha misako na doria nchini. Pindi magari yatakaponunuliwa, yatasambazwa kwenye wilaya zenye uhitaji mkubwa ikiwemo na Wilaya ya Kahama, ahsante.
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved