Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Emmanuel Peter Cherehani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ushetu

Primary Question

MHE. EMMANUEL P. CHEREHANI aliuliza:- Je, Serikali ina mpango gani wa kupeleka gari Ofisi ya Uhamiaji Wilaya ya Kahama ili kuboresha utendaji kazi?

Supplementary Question 1

MHE. EMMANUEL P. CHEREHANI: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa majibu ya Serikali. Wilaya ya Kahama ina halmashauri tatu; Msalala, Kahama pamoja na Ushetu, lakini imekuwa ndiyo lango la nchi jirani; Congo, Burundi, Rwanda na Uganda.

Mheshimiwa Spika, hawa watu hawana gari zaidi ya miaka minne leo, lakini pia wana pikipiki mbili za kudhibiti uhamiaji kitu ambacho ni hatari sana kwa askari wetu.

Mheshimiwa Spika, nataka nipate commitment ya Serikali kwa sababu nimekuwa nikiahidiwa kila mwaka, na mwaka 2024 gari zilipatikana zikapelekwa pale mkoani. Kwa hiyo, hali ya Kahama siyo nzuri, naomba nipate commitment ya Serikali.

Name

Daniel Baran Sillo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Babati Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Spika, nampongeza Mheshimiwa Mbunge kwa ufuatiliaji wa gari la uhamiaji kwa Ofisi ya Kahama. Ni kweli Wilaya ya Kahama ina Halmashauri tatu kwa maana ya Ushetu, Msalala pamoja na Kahama yenyewe.

Mheshimiwa Spika, kama nilivyosema kwenye jibu la msingi, tayari tulishapata kibali kwa ajili ya kununua magari 18. Kwa hiyo, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge katika mgao huu utapata gari kwa ajili ya wilaya yake ya Kahama, ahsante.

Name

Esther Nicholus Matiko

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. EMMANUEL P. CHEREHANI aliuliza:- Je, Serikali ina mpango gani wa kupeleka gari Ofisi ya Uhamiaji Wilaya ya Kahama ili kuboresha utendaji kazi?

Supplementary Question 2

MHE. ESTHER N. MATIKO: Mheshimiwa Spika, Serikali ina mkakati gani wa haraka wa kuhakikisha kwamba inapeleka gari kwenye Ofisi ya uhamiaji Tarime pamoja na Ofisi ya Kipolisi ya Nyamwaga na Tarime ambazo hazina magari kabisa ili kurahisisha utendaji?
SPIKA: Ngoja Mheshimiwa swali ni moja. Uliza mojawapo kati ya hayo uliyouliza.

MHE. ESTHER N. MATIKO: Mheshimiwa Spika, Serikali ina mkakati gani wa haraka wa kuhakikisha kwamba inapeleka gari kwenye Ofisi ya Uhamiaji Tarime ili kurahisisha utendaji, maana hamna gari kabisa? (Makofi)

Name

Daniel Baran Sillo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Babati Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Spika, kama nilivyojibu kwenye swali la msingi, tumeagiza magari 18 na tunaanza na wilaya zile za mpakani kwa ajili ya kuimarisha misako na doria. Kwa hiyo, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwenye mgao huu Wilaya ya Tarime pia itakuwa mojawapo kwa sababu ipo pia mpakani, ahsante sana.