Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
---|---|---|---|---|---|---|
2020-2025 | Session 18 | Sitting 9 | Livestock , Fisheries, Agriculture, Food Security and Cooperatives | Wizara ya Kilimo | 150 | 2025-02-07 |
Name
Leah Jeremiah Komanya
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Meatu
Primary Question
MHE. LEAH J. KOMANYA aliuliza: -
Je, Serikali ina mpango gani wa kutafuta Soko la uhakika la Zao la Alizeti?
Name
David Ernest Silinde
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Tunduma
Answer
NAIBU WAZIRI WA KILIMO alijibu: -
Mheshimiwa Spika, Serikali kwa kushirikiana na wadau inatekeleza mikakati mbalimbali ya kuhakikisha uwepo wa masoko ya uhakika ya mazao ya kilimo ikiwemo zao la alizeti kwa kuhamasisha kilimo cha kibiashara kinachozingatia mahitaji ya soko; kuhamashisha uanzishwaji wa viwanda vya kuongeza thamani ya mazao ya kilimo na kuwaunganisha na wakulima; ukamilishaji wa kanuni za kilimo cha mkataba; na kupitia Mamlaka ya Udhibiti wa Nafaka na Mazao Mchanganyiko (COPRA) kukaa na wadau na kupendekeza bei elekezi ya kununua alizeti kwa kilo pale inapohitajika.
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved