Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
---|---|---|---|---|---|---|
2020-2025 | Session 18 | Sitting 7 | Regional Administration and Local Government Authorities | Ofisi ya Rais TAMISEMI. | 109 | 2025-02-05 |
Name
Silvestry Fransis Koka
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Kibaha Mjini
Primary Question
MHE. SILYVESTRY F. KOKA aliuliza:-
Je, nini hatma ya Shirika la Elimu Kibaha?
Name
Zainab Athuman Katimba
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Answer
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. ZAINAB A. KATIMBA) alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, Shirika la Elimu Kibaha lilianzishwa mwaka 1963 kwa lengo la kuondoa umaskini, ujinga na maradhi ambapo ilisababisha kuanzisha huduma za elimu, afya na uwezeshaji wananchi kiuchumi.
Mheshimiwa Naibu Spika, hata hivyo, tarehe 15 Disemba, 2023, Serikali ilitangaza kuvunja Shirika la Elimu Kibaha ambapo Hospitali ya Tumbi, Kibaha ilitangazwa kuwa Hospitali ya Mkoa wa Pwani.
Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali inaendelea kutafuta namna bora ya kuratibu taasisi zilizo chini ya shirika hilo ili kutoathiri lengo kuu la kuanzishwa kwake.
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved