Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
---|---|---|---|---|---|---|
2020-2025 | Session 18 | Sitting 7 | Regional Administration and Local Government Authorities | Ofisi ya Rais TAMISEMI. | 110 | 2025-02-05 |
Name
Dr. Charles Stephen Kimei
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Vunjo
Primary Question
MHE. DKT. CHARLES S. KIMEI aliuliza:-
Je, ni Shule zipi chakavu katika Jimbo la Vunjo zimewekwa kwenye Mpango wa kufanyiwa ukarabati?
Name
Zainab Athuman Katimba
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Answer
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. ZAINAB A. KATIMBA) alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, katika mwaka 2022/2023, Ofisi ya Rais, TAMISEMI ilifanya tathmini ya mahitaji na hali ya miundombinu ya shule zote za msingi zikiwemo shule za Jimbo la Vunjo. Aidha, kuanzia mwaka 2022/2023 hadi 2023/2024, Serikali imekuwa ikitoa fedha kwa ajili ya ukarabati, ambapo shilingi bilioni 70.39 zimetolewa kwa ajili ya ukarabati wa shule 793 zikijumuisha shilingi bilioni 1.58 zilizokarabati shule za msingi 15 na shule za sekondari tatu zilizopo katika Jimbo la Vunjo.
Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali itaendelea kutenga fedha za ukarabati wa shule chakavu zikiwemo shule za Jimbo la Vunjo kadri ya upatikanaji wa fedha.
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved