Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
---|---|---|---|---|---|---|
2020-2025 | Session 18 | Sitting 7 | Regional Administration and Local Government Authorities | Ofisi ya Rais TAMISEMI. | 111 | 2025-02-05 |
Name
Innocent Edward Kalogeris
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Morogoro Kusini
Primary Question
MHE. INNOCENT E. KALOGERIS aliuliza:-
Je, lini Serikali itajenga vituo vya afya Kata ya Singisa na Bwakila Juu katika Jimbo la Morogoro Kusini?
Name
Dr. Festo John Dugange
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Wanging'ombe
Answer
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE) alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali imeendelea na ujenzi wa vituo vya afya katika Kata za Kimkakati kote nchini, ambapo katika Mwaka wa Fedha 2021/2022, Serikali ilipeleka shilingi bilioni moja kwa ajili ya ujenzi wa Kituo cha Afya cha Kasanga na Mkulazi katika Halmashauri ya Wilaya ya Morogoro ambavyo vimeanza kutoa huduma za wagonjwa wa nje (OPD) na majengo kwa ajili ya huduma za upasuaji wa dharura kwa akinamama wajawazito ambapo ujenzi wake upo hatua ya ukamilishaji.
Mheshimiwa Naibu Spika, Kata ya Singisa ina jumla ya wananchi 14,812, vijiji saba na zahanati moja, hivyo Serikali itafanya tathmini ya Kata hiyo ikiwa inakidhi vigezo vya kata ya kimkakati na mpango wa ujenzi wa kituo cha afya utaandaliwa. Aidha, Kata ya Bwakila juu ina jumla wananchi 6,776, vijiji vitatu na zahanati mbili hivyo haikidhi vigezo vya kuwa na kituo cha afya.
Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali itaendelea kuboresha zahanati zilizopo katika Kata ya Bwakila Juu ili kusogeza huduma za afya karibu na wananchi. Ahsante.
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved