Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
---|---|---|---|---|---|---|
2020-2025 | Session 18 | Sitting 7 | Regional Administration and Local Government Authorities | Ofisi ya Rais TAMISEMI. | 112 | 2025-02-05 |
Name
Vita Rashid Kawawa
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Namtumbo
Primary Question
MHE. SHALLY J. RAYMOND K.n.y. MHE. VITA R. KAWAWA aliuliza:-
Je, lini Serikali itajenga Kituo cha Kisasa cha Mabasi - Namtumbo?
Name
Dr. Festo John Dugange
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Wanging'ombe
Answer
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE) alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali inatambua uhitaji wa kituo cha mabasi katika Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo ili kuboresha huduma za usafiri. Aidha, Halmashauri imefanya tathmini ya ujenzi wa stendi hiyo na kuanza hatua za awali za ujenzi.
Mheshimiwa Naibu Spika, hadi sasa kazi zilizofanyika ni pamoja na kutenga eneo lenye ukubwa wa ekari 3.18 lililopo eneo la Muungano Namtumbo Mjini na kupata hati miliki ya eneo hilo; kuchonga barabara ya kuingia na kutoka; ujenzi wa baadhi ya miundombinu ya awali ambayo ni jengo dogo la abiria, choo cha abiria na mabanda ya biashara ndogondogo. Kazi hizo zimegharimu jumla ya shilingi milioni 34.7
Mheshimiwa Naibu Spika, halmashauri imekamilisha andiko la mradi huo ikiwa ni pamoja na kukamilisha michoro, ramani na makadirio ya gharama. Mradi huo unatarajiwa kugharimu shilingi bilioni 3.5 na hatua inayofuata ni uwasilishaji wa andiko hilo kwa ajili ya upembuzi na kupata fedha kwa ajili ya ujenzi. Ahsante. (Makofi)
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved