Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
---|---|---|---|---|---|---|
2020-2025 | Session 18 | Sitting 7 | Public Service Management | Ofisi ya Rais (Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora) | 113 | 2025-02-05 |
Name
Nancy Hassan Nyalusi
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Primary Question
MHE. SIMON S. LUSENGEKILE K.n.y. MHE. NANCY H. NYALUSI aliuliza:-
Je, Serikali ina mpango gani wa kutoa mafunzo kwa Watumishi wa Umma ili kuendana na kasi ya maendeleo na kuongeza ufanisi?
Name
Deus Clement Sangu
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Kwela
Answer
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, MENEJIMENTI YA UTUMISHI WA UMMA NA UTAWALA BORA alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, katika kuhakikisha watumishi wa umma wanaendelezwa katika taaluma zao ili kuendana na kasi ya maendeleo na kuongeza ufanisi, waajiri wote wanapaswa kuainisha mahitaji ya mafunzo, kuandaa mipango ya mafunzo na kutenga bajeti kila mwaka na kusimamia utekelezaji wake.
Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na waajiri kutenga fedha za mafunzo kwa watumishi wa umma, Serikali pia imekuwa ikipokea fursa za mafunzo ya muda mrefu na mfupi kutoka maeneo mbalimbali ya kimkakati kwa kuzingatia vipaumbele vya Kitaifa kutoka kwa wadau mbalimbali wa Maendeleo wakiwemo Korea, China, India, Indonesia, Japan, Singapore, Misri, Malaysia, Thailand na Bangladesh ambapo kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 zaidi ya watumishi 1,278 walinufaika na fursa hizo. Ninakushukuru.
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved