Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
---|---|---|---|---|---|---|
2020-2025 | Session 18 | Sitting 7 | Public Service Management | Ofisi ya Rais (Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora) | 114 | 2025-02-05 |
Name
Dr. Oscar Ishengoma Kikoyo
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Muleba kusini
Primary Question
MHE. DKT. OSCAR I. KIKOYO aliuliza:-
Je, Serikali ina mkakati gani wa kuwapa posho ya mazingira magumu wafanyakazi hasa walimu wanaopangiwa kazi mikoa ya pembezoni?
Name
Deus Clement Sangu
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Kwela
Answer
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, MENEJIMENTI YA UTUMISHI WA UMMA NA UTAWALA BORA alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali inaendelea kutekeleza mikakati mbalimbali ikiwa ni pamoja na kujenga nyumba za kuishi walimu hususan walimu wa umma na watumishi wa kada za afya katika Mamlaka za Serikali za Mitaa. Pia, ukarabati wa miundombinu ya barabara; kuboresha huduma za jamii kama vile, elimu, afya, maji, nishati ya umeme na mawasiliano ya simu.
Mheshimiwa Naibu Spika, aidha, huduma hizi zinawanufaisha watumishi wa umma wote pamoja na wanaofanya kazi katika mikoa ya pembezoni. Hata hivyo, Serikali haijatoa mwongozo mahsusi wa kulipa posho ya mazingira magumu kwa watumishi wa kada ya ualimu na watumishi wengine wa umma wanaopangiwa vituo vya kazi katika mikoa ya pembezoni kutokana na changamoto mbalimbali zinazoweza kujitokeza katika utekelezaji wake.
Mheshimiwa Naibu Spika, ninashukuru.
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved