Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
---|---|---|---|---|---|---|
2020-2025 | Session 18 | Sitting 7 | Union Affairs | Ofisi ya Makamu wa Rais Mazingira na Muungano | 116 | 2025-02-05 |
Name
Tunza Issa Malapo
Sex
Female
Party
CHADEMA
Constituent
Special Seats
Primary Question
MHE. TUNZA I. MALAPO aliuliza:-
Je, Serikali imefanya Tathmini ya kujua ni Miti mingapi inayopandwa inatunzwa na kukua ili kukabiliana na Mabadiliko ya Tabianchi?
Name
Khamis Hamza Khamis
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Uzini
Answer
NAIBU WAZIRI OFISI YA MAKAMU WA RAIS, MUUNGANO NA MAZINGIRA alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali kupitia Ofisi ya Makamu wa Rais, kwa kushirikiana na Ofisi ya Rais, TAMISEMI, imekuwa ikifanya tathmini ya upandaji miti kwa kila mwaka ili kukabiliana na uharibifu wa ardhi, kuenea kwa hali ya jangwa na ukame na kupambana dhidi ya mabadiliko ya tabianchi.
Mheshimiwa Naibu Spika, katika kipindi cha mwaka 2020/2021 – 2023/2024 tathmini imebainisha kuwa, jumla ya miti milioni 866.7 ilipandwa ambapo kati ya miti hiyo, miti milioni 686.24 ilistawi, sawa na 82.3%. Aidha, katika msimu wa mwaka 2024/2025, Serikali inaendelea kufanya tathmini, ili kubaini idadi ya miti iliyopandwa na iliyostawi kwa maeneo yote nchini.
Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali inaendelea kuhamasisha wananchi na Sekta binafsi kuendelea kupanda miti kwenye maeneo mbalimbali nchini, ili kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi na kutunza mazingira. Aidha, kupitia Bunge lako Tukufu la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, ninaomba kutoa wito kwa jamii nzima ya Watanzania kutumia mvua zinazonyesha kipindi hiki kwa kupanda miti katika maeneo yetu mbalimbali. Nakushukuru.
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved