Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
---|---|---|---|---|---|---|
2020-2025 | Session 18 | Sitting 7 | Energy and Minerals | Wizara ya Nishati | 117 | 2025-02-05 |
Name
Ummy Ally Mwalimu
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Tanga Mjini
Primary Question
MHE. UMMY A. MWALIMU aliuliza:-
Je, Serikali ina mkakati gani wa kuwaunganishia umeme wa gharama nafuu wananchi wa maeneo ya pembezoni yenye sifa za Vijiji, Tanga?
Name
Judith Salvio Kapinga
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Answer
NAIBU WAZIRI WA NISHATI alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, katika kurahisisha upatikanaji wa huduma ya umeme wa bei nafuu kwa maeneo ya pembezoni mwa Jimbo la Tanga Mjini, Serikali kupitia REA, inaendelea kutekeleza Mradi wa Peri-Urban III ambapo Mkandarasi aitwaye OK Electrical anaendelea na zoezi la kuunga wateja kwa baadhi ya mitaa kwa gharama ya shilingi 27,000 ambapo mpaka sasa jumla ya wateja 1,302 wameshaunganishiwa huduma ya umeme.
Mheshimiwa Naibu Spika, aidha, maeneo yaliyosalia yapo kwenye mradi wa kupeleka umeme kwenye vitongoji 15 vya kila Mbunge, ambapo Jimbo la Tanga Mjini litapelekewa umeme kwenye mitaa 15. Serikali inaendelea kuwahimiza wananchi kuunganisha umeme wakati ambapo ujenzi wa miradi unaendelea. Ahsante.
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved